• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

Wazee 25499 Wapatiwa Huduma ya Matibabu Bure Wilayani Magu

Posted on: January 13th, 2019

Halmashauri ya Wilaya ya Magu imefanikiwa kutoa huduma ya matibabu bure kwa Wazee 25499 kwa mwaka 2018, haya yamejiri katika hafla ya kukabidhi vitambulisho vya Matibabu bure kwa wazee wilayani iliyofanyika katika ukumbi wa shule ya sekondari Magu. Mkuu wa Wilaya ya Magu Mheshimiwa Dr. Philemon Sengati akiwa ni Mgeni Rasmi katika hafla hiyo ya kukabidhi vitambulisho vya matibabu bure kwa wazee 300 ambao vimetolewa mwezi huu na Halmashauri ya Magu, amesema kuwa takwimu za mwaka 2018, zinaonesha wazee 18315 wakazi wa Magu walipatiwa huduma ya matibabu bure na 7184 waliapatiwa wakitokea katika wilaya za jirani au nje ya Wilaya ya Magu.

DC Sengati pia amekabidhi fimbo nyeupe tano kwa wasioona, kati ya 426 walemavu wasioona walioko katika Wilaya ya Magu, aidha amesisistiza kuwa Wazee wote wawe na amani katika Serikali hii ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt.John Magufuli iko kwa ajili ya kutetea haki, usawa na kuwakwamua wanyonge “Wazee wangu kwa lolote linalowasibu karibuni sana Ofisi yangu, ya DAS na DED ziko wazi kwa ajili ya kuwasililiza na kuwahudumia, pia ninasisitiza kuwa hakuna haja ya kuendelea kukalishwa kwa muda mrefu kusubiri huduma za matibabu hospital ndiyo maana tunalo dirisha la dawa na chumba cha huduma ya tiba kwa wazee. Lengo ni kuwaenzi wazee wetu kwani hata sisi ni wazee watarajiwa” ‘amesema Dkt. Sengati.

Aidha DC Sengati amesema kuwa faida ya kuwa na Rais Mzalendo anayetekeleza miradi mingi, ahadi za ukweli na anayeziishi ahadi zake za ukweli , “hakika mnaona anavyopambana katika kujenga miradi mikubwa, miundombinu ya barabara, madaraja na reli, moja ya faida ni hii ya ninyi kupatiwa huduma ya matibabu bure! kwa sisi wawakilishi wake tunamuunga mkono na tunamkubali naamini hata ninyi wazee wangu mtakwenda kuwa mawakala wazuri wa Serikali yenu inayowajali bila ubaguzi, aidha wa kidini au kisiasa”.

Naye Mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Magu Lutengano Mwalwiba amesema kuwa huu ni mwendelezo wa Halmshauri kutoa vitambulisho vya matibabu bure kwa wazee," Lengo ni kwamba tunahitaji kila anayefikia umri wa miaka sitini apate kitambulisho na aanze kupatiwa huduma ya mataibabu bure, na Matarajio yetu ni kuona wazee wote mnapatiwa huduma bure kama ilivyo sera ya Serikali, kuwa wazee mnayo haki ya kupatiwa huduma bure na sisi tunaendelea kutekeleza kama ilivyo kusudiwa na Serikali".

Wazee waliopatiwa vitambulisho wamepongeza jitihada za Serikali, “Kweli Serikali imetukumbuka na sisi Wazee kwani huduma ya tiba ni jambo la muhimu sana kwetu wazee, tunampongeza Mheshimiwa Rais kwa kuliona hili na sisi tunamuunga mkono na kwamba bado tunaimani naye na Serikali yake pamoja na Wasaidizi wa Rais, Pia tunamshukuru Dr. Maduhu mganga mkuu wilaya na watoa huduma kwa kutujali pale tunapoenda kupata matitabu katika Hospital ya Wilaya pamoja na vituo vya afya”  amesema Mzee. Helmenegild Mganga.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAGU YAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUENDELEA KUINUA KIUCHUMI KUNDI LA VIJANA

    May 21, 2025
  • MAGU YATENGA MILIONI 92 KUTENGENEZA MADAWATI 1300

    May 21, 2025
  • DC NASSARI AONGOZA KIKAO MAANDALIZI MBIO ZA MWENGE WA UHURU MAGU

    May 21, 2025
  • KILIO CHA MAJI MWAMABANZA KUISHA JUNI 2025

    May 16, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa