• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

WAZAZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO WAHIMIZWA KUWAPELEKA WATOTO SHULE KUANZA MASOMO KWA WAKATI

Posted on: August 19th, 2023

Wakati zoezi la kuripoti wanafunzi wa kidato cha tano kwa mhula mpya wa masomo 2023 likiendelea wazazi wamehimizwa kuwapeleka watoto shule ili waanze masomo kwa wakati kwakua walimu wapo tayari kufundisha na Serikali imeendelea kuboresha miundombinu ambapo Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya kazi kubwa ya kuhakikisha madarasa ya kutosha yanajengwa kila shule.


Wito huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Magu Rachel Kassanda wakati wa  ziara ya kukagua maendeleo ya  kuripoti kwa Wanafunzi wa kidato cha tano wa Shule ya sekondari Magu ambayo hadi sasa imepokea wanafunzi 60 kati ya wanafunzi 152 waliopangiwa kujiunga na Shule hiyo inayopatikana katika kata ya Isandula Wilayani Magu Mkoani Mwanza.

Akizungumza na Wanafunzi wa Shule hiyo DC Kassanda amesema kuwa ni vyema wanafunzi wote wakaanza masomo kwa pamoja ili asiachwe mtu nyuma na kusisitiza kuwa wazazi wa wanafunzi ambao hawajaripoti shule kuongeza juhudi ili kuhakikisha wanafunzi wote wanaripoti shule kwa wakati.


"Niwaombe wazazi waongeze juhudi ili wanafunzi waripoti shule kwani hadi sasa katika shule ya sekondari Magu idadi ya wanafunzi waliofika haifiki hata nusu ya idadi ya jumla ya wanafunzi wote kwani wakiripoti mapema watapata fursa ya kuzoea mazingira na kuanza masomo kwa wakati" amesema .


Katika hatua nyingine DC Kassanda amewataka wanafunzi  kusoma kwa bidii na kufanya vizuri katika mitiani yao ya mwisho pasipo kusikiliza vishawishi ili kuunga mkono uwekezaji wa serikali katika sekta ya elimu na  kuleta maendeleo ya Taifa.


Kwa upande wake Makamu Mkuu wa Shule ya Sekondari Magu Mathew Kabuta ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa ujenzi wa miundombinu kwaajili ya wanafunzi wa kidato cha tano .

Akizungumza kwa niaba ya wanafunzi wa kidato cha tano shule ya Sekondari Mgu , Gideon R. Ayo amesema wameridhishwa na mazingira ya shule kwani ina miundombinu yote na huduma muhimu kama maji , umeme na chakula inapatikana hivyo amewahamisisha wanafunzi wenzake kuripoti shule ili waanze masomo pamoja.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WADAU WA SANAA MAGU WATAKIWA KUJISAJILI BASATA

    May 07, 2025
  • INEC YARIDHISHWA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA MAGU

    May 03, 2025
  • DC Magu:Wazazi pelekeni watoto wapate chanjo ya polio

    April 30, 2025
  • WAANDISHI, WAENDESHA BVR 136 WALA KIAPO MAGU

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa