• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

WATENDAJI KATA, VIONGOZI WA DINI MAGU WAPEWA DARASA UELIMISHAJI JAMII KUHUSU SARATANI YA MATITI

Posted on: September 23rd, 2025

Watendaji wa kata, wahudumu wa afya ngazi ya jamii na viongozi wa dini kutoka halmashauri ya wilaya ya Magu, wametakiwa kutumia nafasi zao kuelimisha jamii namna ya kufanya uchunguzi wa awali wa saratani ya matiti lakini pia kuwa na utamaduni wa kwenda hospitali kufanya uchunguzi ugonjwa huo walau mara moja kwa mwaka.

Wito huo umetolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu, Mohamed Kyande wakati akifungua mafunzo ya siku moja kuhusu uchunguzi wa saratani ya matiti kwa watendaji kata, wahudumu wa afya ngazi ya jamii, viongozi wa dini kutoka Magu.

Mafunzo hayo yaliyotolewa leo Jumanne na Shirika la kimataifa la Jhpiego kwa kushirikiana na Pfizer Foundation katika ofisi za Halmashauri Magu zilizopo Ilungu, yamelenga kuwawezesha washiriki kuhamasisha jamii kufanya uchunguzi wa saratani ya matiti mara kwa mara.

“Uchunguzi wa mapema ni kinga kubwa ya maisha, kwani saratani ya matiti ikigundulika mapema inatibika,” alisisitiza Kyande.

Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Wilaya ya Magu, Dk. Mhana Raphael amesema saratani ya matiti bado ni changamoto kubwa katika jamii na imekuwa ikisababisha asilimia 23 ya vifo vitokanavyo na magonjwa hayo ya saratani huku saratani ya shingo ya kizazi ikiongoza kwa asilimia 25.

“Niwashukuru Jhpiego kwa sababu wanawajengea uelewa wataalam wetu kwa sababu ili tuifikie jamii kwa urahisi, tunatumia viongozi wa dini, watendaji wa kata ili kila mmoja akatimize wajibu. Tunataka kuona kila mwanajamii anajichunguza na anapima mapema, ili kupunguza athari na kuokoa maisha. Nitoe wito kwa washiriki wa mafunzo haya kwa sababu ndiyo daraja letu la kufikisha elimu hiyo kwa wananchi,” alisema.

Mradi huu unafadhiliwa na Pfizer Foundation kupitia Jhpiego na unatarajiwa kudumu kwa kipindi cha miaka mitatu mkoani Mwanza.

Aidha, washiriki wa mafunzo wameahidi kushirikiana na wataalamu wa afya ili kuifikisha elimu ngazi ya jamii, kuhimiza wananchi kujitokeza kwa wingi kufanya uchunguzi wa saratani ya matiti na hivyo kupunguza vifo vinavyosababishwa na ugonjwa huo.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WATENDAJI KATA, VIONGOZI WA DINI MAGU WAPEWA DARASA UELIMISHAJI JAMII KUHUSU SARATANI YA MATITI

    September 23, 2025
  • RC MWANZA AWAALIKA WALIOKOSA ELIMU RASMI KUJIUNGA NA MPANGO WA ELIMU YA WATU WAZIMA

    September 15, 2025
  • UTEKELEZAJI SHUGHULI ZA LISHE MAGU WAVUKA 100%

    September 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKEWA MAGU WAZINDUA MIRADI YA BIL. 2

    August 27, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa