• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

WAANDIKISHAJI UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA WAASWA KUWA WELEDI, KUZINGATIA SHERIA

Posted on: October 8th, 2024

MAOFISA uandikishaji katika daftari la uchaguzi wa serikali mitaa wametakiwa kuzingatia kanuni na sheria za uchaguzi huo pamoja na kuwa waadilifu ili kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Wito huo umetolewa jana tarehe 8 Oktoba, 2024 mjini Magu mkoani Mwanza na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu, Mohamed Ramadhan Kyande wakati akiwaapisha waandikishaji hao.

Alisema kiapo walichoapa waandishikishaji hao ndio kitanzi chao hivyo wanapaswa kuzingatia maadili na sheria za uchaguzi huo ili kuondoa malalamiko yoyote yanayoweza kujitokeza.

“Niwapongeze kushiriki kwenye semina, uteuzi wenu umepitia hatua mbalimbali za upembuzi hivyo mmepitia kwenye tanuru la moto kwelikweli, lakini pia walioachwa sio kwamba hawakuwa na uwezo bali nafasi ni chache hivyo tukafanya kazi kwa uweledi na uadilifu mkubwa,” alisema.

Naye Afisa Uchaguzi wilaya ya Magu, Mwagala Masunga alisema zoezi la kuandikisha wapiga kura uchaguzi huo litaanza tarehe 11 hadi 20 Oktoba mwaka huu huku kampeni zikitarajiwa kuanza tarehe 20 hadi 26 Novemba mwaka huu.

Aidha, aliwaonya waandikishaji hao kuandikisha wananchi wote kwenye vitongoji vya bila kujali itikadi zao za vyama.

“Tushirikiane kukamilisha zoezi hili. Mkihitaji maelekezo msisite kuwasiliana na ofisi yangu,” alisema.

Alisema uchaguzi huo utafanyika katika mamlaka mji mdogo wa Magu Pamoja na wilaya ya Magu ambapo kwa ujumla kuna vijiji 82 na vitongoji 508.

Alisema viongozi wanaochaguliwa katika ngazi hizo ni wenyeviti wa vijiji, wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji, wenyeviti wa mitaa, wajumbe wa kamati za mitaa na wenyeviti wa vitongoji.

Zoezi la kujiandikisha litazinduliwa rasmi tarehe 11 Oktoba, 2024 na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ilihali uchaguzi huo wa Serikali za Mitaa, unatarajiwa kufanyika tarehe 27 Novemba mwaka huu, kote nchini.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAGU YAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUENDELEA KUINUA KIUCHUMI KUNDI LA VIJANA

    May 21, 2025
  • MAGU YATENGA MILIONI 92 KUTENGENEZA MADAWATI 1300

    May 21, 2025
  • DC NASSARI AONGOZA KIKAO MAANDALIZI MBIO ZA MWENGE WA UHURU MAGU

    May 21, 2025
  • KILIO CHA MAJI MWAMABANZA KUISHA JUNI 2025

    May 16, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa