• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

Mkuu wa Wilaya ya Magu Aitaka Jamii Kusimamia Malezi na Makuzi ya Watoto

Posted on: June 21st, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Magu Mwalimu Khadija  Nyembo ameitaka Jamii kuhakikisha inasimamia malezi na makuzi ya watoto vizuri wakati Taifa likiwa linaekea katika Uchumi wa Viwanda.  Ameyasema hayo leo Juni 20, 2018 katika kilele cha Maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika Wilayani Magu, yaliyofanyika katika Kata ya Itumbili, ambapo alikuwa mgeni Rasmi katika maamizisho hayo. Nyembo ameitaka jamii kuhakikisha kuwa Watoto wetu wanakua na kulelewa vizuri ili waweze kuielewa dhamira njema ya Serikali ya awamu ya tano iliyoamua kuamsha viwanda katika Taifa kwa lengo la kukuza ajira na stadi za kazi kwa kuifanya Tanzania kuwa Taifa la Viwanda hivyo maadili mema yanahitajika ili kuwandaa watalaam wenye weledi na Uzalendo.

Awali Watoto walisoma Risala kwa Mkuu wa Wilaya iliyaoanisha changamoto zinazowakabili watoto wilayani magu, ikiwemo Ulinzi wa Mtoto, kukatishwa masomo, Kuletekezwa na wazazi, Ukosefu wa mabaraza ya watoto, Vilabu vya watoto Shuleni, Ajira za utotoni, Ukosefu wa maeneo ya michezo, Vitendo vya udhalilishaji, unyanyasaji vinavyopelekea kwa watoto kushindwa kufikia ndoto za maisha yao ya baadaye.

Naye Mgeni Rasmi Mhe.Khadija Nyembo amewahakikishia wananchi na watoto kwa ujumla kuwa, Serikali haitafumbia macho vitendo vyovyote, au mtu yeyote atakayejaribu kuharibu au kukiuka sheria na haki ya mtoto. Sheria itachukua mkondo wake dhidi ya mtu huyo. Na kwamba anahitaji kuona maadili mema kwa watoto yakidumishwa na kuheshimiwa katika jamii. Pia ametoa mwelekeo kuwa Serikali tayari imeshaanza utaratibu wa Kuanzisha mabara ya watoto kuanzia ngazi ya Kijiji hadi Wilaya, Vikundi vya ulinzi wa mtoto, Utoaji wa elimu ya haki ya mtoto na utoaji taarifa pale panapotokea ukiukaji wa haki za mtoto program hii Serikali inashirikiana na Shirika la watoto Duniani (UNICEF).

MKuu wa Wilaya pia amewashukuru Wananchi, Wazazi/Walezi na Vituo vya kulelea watoto waliohudhuria na kuaonesha shughuli mbalimbali za Stadi kazi wanazofundisha kwa watoto, Compassion AICT-Magu, Ilungu, Lugeye, Nyanguge, PF(Pathfinder-SDA Magu) na ELCT-Magu ambao wameonesha stadi za ufundi mbalimbali wanazofundisha kama Ufundi Umeme, Ufundi Ujenzi, Ufundi Seremala, Ushonaji na ufumaji, Ushonaji viatu, Uokaji wa mikate na maandazi,” hii ndiyo Tanzania ya viwanda tunayoitaka” Nyembo alishuwakuru na kuwahakikishia kuwa Serikali itaendelea kuwapa ushirikiano kwa mfano mzuri walioonesha kuunga mkono juhudi za Serikali ya awamu ya tano kuelekea Uchumi wa Viwanda na kauli mbiu ya mwaka huu inayosema "KUELEKEA UCHUMI WA VIWANDA TUSIMUACHE MTOTO NYUMA" Amesisitiza Nyembo.

Naye Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Magu, Bwana Fundikira Said ameitaka jamii kuendelea kushirikiana na Watoto kwa karibu zaidi katika kuhakikisha kuwa tunabaini na kutatua changamoto au matatizo ya watoto wetu kwa wakati, pia kuhakikisha kuwa jukumu la kulea mtoto ni la mzazi au mlezi hivyo, hatuhitaji kuona watoto wakikatishwa masomo, aidha kwa kuozeshwa, au kuzurura mitaani.

Afisa Maendeleo Bi,Shida Misana amefafanua kuwa dhana ya Viwanda ni fikra zaidi ya majengo. Hivyo akatoa wito kwa jamii kushiriki kikamilifu katika kuwalea watoto kwa kuwapa elimu zaidi kuwa VIWANDA ni kuongeza thamani ya kile unachozalisha, Pia amesisitiza kuwa Elimu ya Kujitegemea na Ufundi inahitaji kuongezewa kasi ya kufundishwa shuleni ili kuwaandaa watoto katika kuelekea Tanzania ya Viwanda.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WADAU WA SANAA MAGU WATAKIWA KUJISAJILI BASATA

    May 07, 2025
  • INEC YARIDHISHWA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA MAGU

    May 03, 2025
  • DC Magu:Wazazi pelekeni watoto wapate chanjo ya polio

    April 30, 2025
  • WAANDISHI, WAENDESHA BVR 136 WALA KIAPO MAGU

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa