• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

MBUNGE KISWAGA AMSHUKURU RAIS DKT. SAMIA KUIDHINISHA MIL 384 UJENZI WA SHULE YA KIGANGAMA

Posted on: December 22nd, 2023

Mbunge wa jimbo la Magu Boniventura Kiswaga amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuidhinisha shilingi Milioni 584 kwaajili ya ujenzi wa shule mpya ya sekondari Kigangama katika Kijiji cha Kigangama kata ya Kitongosima Wilayani Magu ambayo ujenzi wake upo katika hatua za mwisho na itarajiwa kupokea wanafunzi katika mhula mpya wa masomo 2024-2025.

Mbunge Kiswaga ametoa shukrani hizo wakati wa ziara ya kamati ya mfuko wa jimbo kwaajili ya kukagua miradi iliyopelekewa fedha kwa mwaka wa fedha 2022-2023 kwa lengo la kuchochea maendeleo ya miradi mbalimbali iliyoanzishwa na wananchi katika Jimbo la Magu ambapo mfuko wa jimbo ulipeleka shilingi milioni 5, 440, 000 kwaajili ya kuchangia zoezi la ununuzi wa tofali za ujenzi wa shule hiyo.


Akizungumza wakati wa ziara hiyo mbunge Kiswaga amesema shule hiyo inayojengwa kupitia mradi wa kuboresha Elimu ya Sekondari ( SEQUIP) itasaidia kutatua changamoto ya wananfunzi kutembea umbali mrefu ambapo wanafunzi wa kata hiyo wanatembea takribani KM 7 kwenda katika shule ya sekondari Lugeye.


" Tunamshukuru sana Rais Dkt. Samia kwa kudhinisha pesa kwaajili ya ujenzi wa shule hii na kuona uhitaji wa wananchi kuhitaji shule katika kijiji hiki kwani wanafunzi wengi walikua wanaishia njiani kutokana na umbali hivyo tunamshukuru sana Mh. Rais kwa kuliona hili".


Aidha Kiswaga amebainisha kuwa fedha za mfuko wa jimbo zipo kwa lengo la kusaidia miradi ya wananchi iliyoanzishwa kwa manufaa ya Taifa ili iweze kukamilika hivyo akawahimiza wasimamizi wa miradi kusimamia vizuri na kuhakikisha miradi hiyo inakamilika ili fedha za mfuko wa jimbo zitumike kama ilivyokusudiwa .

Kwa upande wake Afisa Mipango wa Wilaya ya Magu Pastory Mkaruka amesema katika ziara hiyo wametembelea miradi mbalimbali na kuona thamani ya fedha zilizotolewa na mfuko wa jimbo zilizvyotumika katika kuchochea maendeleo ya miradi mbalimbali iliyoanzishwa na wananchi.


Aidha alimshukuru Mbunge Kiswaga kwa jitihada za kuhakikisha fedha za mfuko wa jimbo zinapatikana na kuchochea miradi mbalimbali iliyoanzishwa na wananchi.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAGU YAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUENDELEA KUINUA KIUCHUMI KUNDI LA VIJANA

    May 21, 2025
  • MAGU YATENGA MILIONI 92 KUTENGENEZA MADAWATI 1300

    May 21, 2025
  • DC NASSARI AONGOZA KIKAO MAANDALIZI MBIO ZA MWENGE WA UHURU MAGU

    May 21, 2025
  • KILIO CHA MAJI MWAMABANZA KUISHA JUNI 2025

    May 16, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa