• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

DC LAWUO AWAPA POLE FAMILIA ILIYOPOTEZA 3 KWA AJALI YA MOTO MAGU

Posted on: January 16th, 2026

MKUU wa Wilaya ya Magu, Jubilate Lawuo ameitembelea familia ya Mzee Shadrack Ntagala (66) iliyopata ajali ya moto na kuipa pole huku akiwasisitiza wananchi kuchukua tahadhari ya matumizi ya vifaa vya umeme na kutoa taarifa haraka tatizo linapotokea.

Katika ajali hiyo ya moto iliyotokea saa sita usiku wa kuamkia leo maeneo ya mtaa wa National kata ya Magu Mjini wilayani Magu, jumla ya watu watatu wa familia hiyo wamefariki dunia huku baba wa familia akinusurika.

Kwa mujibu wa Mkuu wa Zimamoto na Uokoja Wilayani Magu, Inspekta Gaston Tibulebwa katika nyumba hiyo iliyokuwa na watu wanne, waliofariki ni Mwakebeta Mathew (62) ambaye ni mke wa Ntagala, Liberate Ngwata (40) ambaye ni dada wa Ntagala pamoja na Neema Festo Kizinga (18) ambaye ni mjukuu na mwanafunzi wa kidato cha tatu Magu Sekondari.

Amesema mzee Ntagala amenusurika baada ya kuokolewa na kijana aliyekuwa amelala nyumba ya jirani. Kijana huyo alifanikiwa kuvunja mlango wa nyumba hiyo na kumtoa mzee huyo ambaye sasa anapatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda Bugando jijini Mwanza.

Awali DC Lawuo akizungumza na wanafamilia pamoja na wananchi waliofika kuomboleza, mbali na kuwapa pole wafiwa, amelipongeza jeshi la zimamoto na uokoaji wilaya ya Magu kwa kufika kwa wakati na kusaidia kuzima moto huo usilete madhara zaidi.

“Ndugu zangu Wana-Magu tunatakiwa kuwa makini na mali zetu, ukiona tukio lolote tupeane taarifa mapema ili uharibifu mkubwa kama huu usitokee.

 

“Inspekta Gaston amekuwa akitoa namba za simu kwa wananchi wote ili kunapotokea tukio wakati wowote mtoe taarifa, lakini pia niwaombe kuchunguza vifaa vya umeme tunavyovitumia, tusitumie cable moja kwenye matumizi ya vifaa vyote vya ndani, ikizidiwa inapata joto na kuungua,”

Aidha, akielezea tukio hilo dada wa Ntagala, Mwinjilisti Marry Yona amesema taarifa za tukio hilo amezipata saa 10 usiku wa kuamkia leo wakati akiwa kwenye shughuli zake katika kata jirani ya Nyanguge.

Akielezea hali ya kaka yake amesema, majeruhi huyo anaendelea kupatiwa matibabu katika hospitali ya rufaa kanda Bugando hivyo wanaendelea kuangalia hali yake ndipo watajua taratibu za mazishi ya wapendwa wao ambao miili yao imehifadhiwa katika mochwari hospitali ya wilaya ya Magu.

Naye kijana Mashaka Mabula ambaye ndiye aliyekuwa wa kufika kwenye tukio na kumuokoa Mzee Ntagala, amesema alijulishwa kuhusu tukio hilo na mama mmoja wa jirani.

“Alikuja kunigongea na kuniambia kuna moto unawaka kwenye nyumba wa baba wa familia. Nikaenda kuvunja mlango nikakuta mzee yupo mlangoni nikamtoa ndipo nikaanza kuzima moto kwa kuunganisha mpira wa maji kwenye bomba lililo hapa nje,” amesema na kuongeza kuwa baada ya muda kidogo ndipo askari wa zimamoto na uokoaji walikuja na kusaidia kuzima moto huo.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • DC LAWUO AWAPA POLE FAMILIA ILIYOPOTEZA 3 KWA AJALI YA MOTO MAGU

    January 16, 2026
  • BARAZA LA WAFANYAKAZI MAGU LAPATA MAKATIBU WAPYA

    January 14, 2026
  • WFANYABIASHARA WA MASOKO MAGU WATAKIWA KUTUNZA MAZINGIRA KWA KUFANYA USAFI

    December 19, 2025
  • TALGWU YASISITIZA NIDHAMU, WELEDI NA UTIIFU KWA WANACHAMA WAKE

    December 18, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa