• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

MAGU YAADHIMISHA SIKU YA LISHE KITAIFA, WAZAZI WAHIMIZWA KUUNGA MKONO ZOEZI LA KUCHANGIA CHAKULA SHULENI

Posted on: October 30th, 2023

Wazazi Wilayani Magu wamehimizwa kutambua  umuhimu wa chakula kwa afya ya mtoto, kuwa ndicho kinachojenga akili, mwili na saikolojia ya mtoto, hivyo wameombwa  kuchukulua  umuhimu mkubwa jambo hilo kwa kuunga mkono zoezi la kuchangia chakula shuleni kwa ajili ya umuhimu wa Lishe Bora na ufaulu wa watoto.


Wito huo umetolewa na Katibu Tawala wa Wilaya ya Magu Jubilate win Lawuo wakati wa maadhimisho ya siku ya Lishe Kitaifa yenye kauli mbiu " Lishe Bora kwa Vijana Balehe, Chachu ya Mafanikio Yao" kwa Wilaya ya Magu ambayo yaliambatana na uzinduzi wa kampeni ya lishe kwa vijana balehe yaliyofanyika katika shule za ya Msingi Nyalikungu Leo Jumatatu Oktoba 30, 2023.


Akizungumza wakati wa maadhimisho hayo Katibu Tawala huyo amesema suala la chakula ni muhimu sana ba lazima lizingatiwe ili wanafunzi waweze kusoma kwa ufanisi wawapo shuleni.

" Hii itasaidia kuinua ufaulu wa wanafunzi na kuimarisha mahudhurio yao kwani wanafunzi wengi wamekua wakitoroka shuleni kwaajili ya kwenda nyuma kula chakula hivyo ni vyema wazazi tukaona umuhimu na kuunga mkono suala hili" amesema


Aidha Katibu Tawala Lawuo amewahimiza wananchi kuzingatia mlo kamili na kuepuka  ulaji wa vyakula  vyenye  mafuta, sukari, na chumvi kwa wingi mfano Chipsi, soda, Pizza, Biskuti, keki, na mikate ya unga mweupe,soda, juisi zilizoongezewa sukari, na vyakula vya kukaanga ikiwemo mihogo, viazi, nyama kwani itasaidia Kuepuka unene/uzito kupita kiasi, magonjwa ya moyo, kiharusi, shinikizo la juu la damu, saratani, kisukari na ugonjwa wa figo sasa na baadae.



Kwa upande wake Afisa Lishe Wilaya ya Magu Bi Magdalena G. Lema amesema  Magu ni miongoni mwa halmashauri nchini zinazotekeleza afua za lishe ili kutokomeza/Kupunguza changamoto mbalimbali za lishe kwa mama mjamzito, watoto chini ya miaka mitano

"leo tunazindua rasmi mkakati wa kutokomeza/kupunguza changamoto za lishe kwa vijana balehe ili kufikia kiwango ambacho si tatizo katika jamii kwa utaratibu wa kutoa elimu na kupima hali za lishe za vijana balehe(miaka 5-19)" amesema


Kuhusu mafanikio yaliyopatikana tangu kuanzishwa kwa mpango wa Lishe Kitaifa Wilaya ya Magu imfanikiwa kupunguza hali ya ukondefu kwa watoto wa chini miaka mitano kutoka 3.5% Hadi 2.8% .

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WADAU WA SANAA MAGU WATAKIWA KUJISAJILI BASATA

    May 07, 2025
  • INEC YARIDHISHWA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA MAGU

    May 03, 2025
  • DC Magu:Wazazi pelekeni watoto wapate chanjo ya polio

    April 30, 2025
  • WAANDISHI, WAENDESHA BVR 136 WALA KIAPO MAGU

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa