• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

Kiongozi mbio za mwenge aweka jiwe la msingi Kituo cha Afya Nyanguge

Posted on: October 13th, 2024

Na Mwandishi Wetu, Mwanza

Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru, Godfrey Mzava ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa wodi ya wazazi katika Kituo cha Afya Nyanguge wilayani Magu mkoani Mwanza na kueleza kuridhishwa na utekelezaji wa mradi huo.

Kiongozi huyo wa mbio za Mwenge wa uhuru ameweka jiwe hilo la msingi mwishoni mwa wiki baada ya kukagua mradi huo na kuridhishwa na ujenzi wake ambao ulianza tarehe 25 Februari mwaka 2022.

Awali Mratibu wa Mwenge wa uhuru Wilaya ya Magu, Peter Mujaya, alisema utekelezaji wa mradi huo hadi kukamilika Juni 2024/2025, unakadiriwa kutumia jumla ya Sh milioni 250, fedha kutoka mapato ya ndani ya Halmashauri.

“Mpaka sasa Halmashauri imeshatoa jumla ya Sh milioni 150 kati ya fedha hizo kiasi cha Sh milioni 123 kimetumika kununua vifaa vya ujenzi na kulipa mafundi ujenzi. Mpaka sasa ujenzi upo katika hatua ya ukamilishaji, amesema.

Akizungumzia mradi huo, Mzava aliipongeza halmashauri hiyo kwa kuwekeza nguvu katika kuboresha huduma ya mama na mtoto hasa ikizingatiwa ni makundi ambayo yana uhitaji mkubwa wa afya bora kwa kizazi cha baadae.

Aidha, akizungumzia mapambano dhidi ya ugonjwa wa malaria katika wilaya ya Magu, Mzava aliipongeza halmashauri hiyo kwa kufanikiwa kupunguza maambukizi ya ugonjwa huo kutoka asilimia 18.9 mwaka 2023 hadi asilimia 12.7 mwaka 2024.

Pamoja na jitihada hizo alitoa wito kwa jamii kuhakikisha wanatumia dozi za malaria ipasavyo bila kukatisha na kutumia dawa za kienyeji ili kuunga mkono juhudi za serikali katika mapambano dhidi ya ugonjwa huo.

Kiongozi huyo wa mbio za Mwenge wa uhuru pia alitoa wito kwa wilaya hiyo kuendelea kutoa elimu Pamoja na kudhibiti maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi (VVU) ili kulinda afya za wananchi wa wilaya hiyo.

Pia aliipongeza wilaya ya Magu kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa masuala ya lishe kuendelea kusimamia kikamilifu suala la lishe bora kwa wananchi wote kwa kuhakikisha kuwa inapunguza tatizo la udumavu kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano.

Alitoa wito kwa jamii kuzingatia umuhimu wa unyonyeshaji maziwa ya mama pekee kwa kipindi cha miezi sita ya mwanzo ili kuwa na jamii yenye afya imara katika kutekeleza shughuli za kijamii na kiuchumi.

Kwa upande wake, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk. Stagomena Tax alisema ujenzi wa wodi hiyo ya wazazi ni muendelezo wa hlamshauri hiyo kuboresha huduma za afya.

“Hakuna maendeleo bila afya, hivyo natoa wito kwa wananchi wenzangu kutunza miundombinu ya mradi huu kwa sababu mbali na huduma za afya itatufungulia pia milango ya kiuchumi,’ alisema.

Pamoja na mambo mengine alitoa wito kwa wananchi kwenda kujiandikisha katika daftari la uchaguzi wa serikali za mitaa lililofunguliwa tarehe 11 Oktoba mwaka huu hadi tarehe 20 Oktoba ili kumchagua kiongozi atakayeungana na serikali kuwaletea maendeleo.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WADAU WA SANAA MAGU WATAKIWA KUJISAJILI BASATA

    May 07, 2025
  • INEC YARIDHISHWA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA MAGU

    May 03, 2025
  • DC Magu:Wazazi pelekeni watoto wapate chanjo ya polio

    April 30, 2025
  • WAANDISHI, WAENDESHA BVR 136 WALA KIAPO MAGU

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa