• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

KICHEKO SHULE MPYA BUNDILYA IKIANZA KUTOA HUDUMA

Posted on: July 21st, 2025

HATIMAYE Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu, Mohamed Ramadhani amefungua rasmi utoaji huduma katika shule mpya ya sekondari Bundilya iliyopo katika Kijiji cha Bundilya kata ya Kahangara wilayani humo.

Shule hiyo iliyojengwa kwa gharama ya Sh milioni 584.2 fedha za Mradi wa Kuboresha Elimu ya Sekondari (SEQUIP), ujenzi wake ulianza Septemba mwaka jana na kukamilika Juni 30, mwaka huu.

Akizungumza na wananchi pamoja na baadhi ya wanafunzi waliohudhuria hafla ya ufunguzi huo wa utoaji wa huduma shuleni hapo, Mkurugenzi huyo amewapongeza wananchi wa Kijiji hicho cha Bundilya kutokana na nguvu kazi waliyoitoa hadi kufanikisha ujenzi wake.

“Mwaka jana tulikuwa pamoja hapa na viongozi wote tukachimba msingi pamoja. Wananchi walichangia mchanga tripu 90 sio ndogo! pia walichangia maji tangu ujenzi unaanza. Ushirikiano huu maeneo mengine hatuupati hivyo tunawashukuru sana,” amesema.

Pamoja na mambo mengine ameiasa jamii kushirikiana kuhakikisha watoto wao wanasoma ikiwamo kuweka utaratibu maalumu wa uchangiaji wa chakula na kuhakikisha kunakuwepo an mazingira rafiki ya watoto kusoma.

Awali akisoma taarifa ya ujenzi wa shule hiyo, Mwalimu Mkuu wa Sekondari ya Kahangara, James Ndega amesema lengo la mradi huo kuongeza fursa za upatikanaji wa elimu ya sekondari kwa kuwapunguzia umbali wanafunzi na kupunguza msongamano katika shule ya sekondari Kahangara na kuhakikisha wanafunzi wanapata elimu bora wawapo shuleni.

“Mradi unaenda kupokea wanafunzi 79 wa kidato cha kwanza kutoka shule mama ya Kahangara sekondari, miongoni mwao 35 ni wasichana na 44 ni wavulana. Mradi ulitengeneza ajira 57.

“Pia imejengwa miundombinu 11 inayojumuisha madarasa manne na ofisi mbili, jengo la maabara ya fizikia, baiolojia, kemia, jengo la utawala, maktaba, kompyuta na vyoo matundu nane ambapo manne ya wavulana na manne wasichana pamoja na tanki la maji kuvuna maji ya mvua,” amesema.

Naye Afisa Elimu Sekondari Magu, Beatrice Balige amesema kukamilika kwa shule hiyo kumeongeza idadi ya shule katika wilaya ya Magu kufikia 42 za Sekondari.

“Shule tayatri imepata usajili tarehe 3 Julai mwaka huu kwa namba 7008. Tunashukuru kwa ushirikiano mkubwa tuliopata kutoka kwa wananchi na mafundi waliofanya kazi hii kwa uweledi mkubwa.

“Sasa tumewapokea wanafunzi tusipowapa maarifa ya kutosha jitihada hizi zitakuwa zimepotea. Tunahitaji mzazi ufanye sehemu yako na jamii vivyo hivyo.  Wazazi tuna wajibu wa kuhakikisha wanafunzi wetu wanaenda kwa mienendo mizuri ili kufikia malengo yao,” amesema.

Aidha, baadhi ya wazazi wameishukuru Serikali kwa ujenzi wa shule hiyo hasa ikizingatiwa inakwenda kupunguza changamoto ya watoto kutembea umbali mrefu kufuata huduma katika shule ya sekondari Kahangara.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • KICHEKO SHULE MPYA BUNDILYA IKIANZA KUTOA HUDUMA

    July 21, 2025
  • KICHEKO SHULE MPYA BUNDILYA IKIANZA KUTOA HUDUMA

    July 21, 2025
  • TAWLA YATAMBULISHA MRADI WA KUTOKOMEZA UKATILI WA KIJINSIA MAGU

    July 18, 2025
  • KWAHERI JOSHUA NASSARI, KARIBU DC LAWUO

    July 16, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa