• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

KAMATI YA USHAURI MAGU YAPITIA NA KUJADILI RASIMU YA BAJETI KWA MWAKA 2025/2026

Posted on: January 23rd, 2025

KAMATI ya Ushauri ya Wilaya ya Magu (DCC) imepitia na kujadili mapendekezo ya rasimu ya mpango na bajeti ya halmashauri kwa mwaka 2025/2026 ambayo imependekeza kuidhinishwa jumla ya Sh. 64.2 bilioni kutoka vyanzo mbalimbali na kutoka ruzuku ya Serikali Kuu.

Akiwasilisha rasimu ya bajeti hiyo leo Alhamisi mbele ya Mwenyekiti wa kamati hiyo ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Magu, Joshua Nassari, Afisa Mipango wa wilaya, Pastory Mukaruka amesema bajeti hiyo inalenga kuzingatia vipaumbele vinne.

Mukaruka ambaye aliwasilisha rasimu hiyo kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu, Mohamed Ramadhani, ametaja vipaumbele hivyo kuwa ni kuimarisha utawala bora unaohusisha kusikiliza, kupokea na kushughulikia kero za wananchi na ulipaji wa fidia ya ardhi kwa wananchi waliotwaliwa maeneo yao kwa ajili ya shughuli za umma.

Kipaumbele cha pili ni kuboresha upatikanaji wa huduma za kijamii kwa makundi yote, kuboresha hali ya Lishe na ukamilishaji wa miundombinu ya afya, kuendeleza ujenzi wa Kituo cha Afya Nyanguge, kukamilisha ujenzi wa zahanati 6, kituo 1 cha Afya na nyumba 2 za Watumishi wa kada ya Afya na kuboresha mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji shuleni.

“Tatu ni kuimarisha na kuongeza wigi wa ukusanyaji wa mapato ya ndani ili kuongeza ubora na utoaji wa huduma za kijamii na kiuchumi kutoka bilioni 4.73 mwaka 2024/2025 hadi kufikia bilioni 5.23 ifikapo mwaka 2026.

“Kuendeleza ujenzi wa stendi ya kisasa ya Wilaya eneo la Ilungu na stendi ya magari madogo (Hiance) kona ya Kayenze, kujenga ukumbi wa mikutano wa Halmashauri, kupandisha hadhi mnada wa Nyanguge kuwa mnada wa upili,” amesema.

Kipaumbele cha mwisho amesema ni kuiwezesha jamii katika uboreshaji wa masuala ya jinsia na ustawi wa jamii, kuinua uchumi wa makundi maalumu, kuwezesha kutoa mikopo wa 10% kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.

Aidha, amezema katika kipindi cha mwaka 2024/2025 Halmashauri ilipanga kukusanya na kutumia jumla ya Sh bilioni 56.9 kutekeleza Shughuli mbalimbali za maendeleo na matumizi ya kawaida.

Awali akifungua kikao hicho, DC Nassari amesema lengo  kushirikisha wadau wote muhimu wa halmashauri hiyo kushiriki kikamilifu katika upangaji na kupata ufafanuzi wa mapato na matumizi ya wilaya hiyo.

Pamoja na mambo mengine amesema katika bajeti inayoishia mwaka huu wa fedha 2024/2025, halmashauri hiyo imefanikiwa kutekeleza miradi mbalimbali ikiwamo kuboresha makusanyo hadi kutoka asilimia 57 hadi kufikia asilimia 97.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WADAU WA SANAA MAGU WATAKIWA KUJISAJILI BASATA

    May 07, 2025
  • INEC YARIDHISHWA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA MAGU

    May 03, 2025
  • DC Magu:Wazazi pelekeni watoto wapate chanjo ya polio

    April 30, 2025
  • WAANDISHI, WAENDESHA BVR 136 WALA KIAPO MAGU

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa