• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

KAMATI YA USALAMA, WATENDAJI KATA MAGU WAPIGWA MSASA KUHUSU UTAWALA BORA

Posted on: March 11th, 2025

Wizara ya Katiba na Sheria imetoa mafunzo ya utawala bora na uraia kwa kamati ya usalama ya wilaya ya Magu, wakuu wa idara mbalimbali za halmashauri na watendaji wa kata wilaya hiyo ili kuwakumbusha kuzingatia mipaka katika utumishi na misingi ya utawala bora pamoja na kukuza utaifa na uzalendo miongoni mwao.

Akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo hayo jana Jumatatu wilayani Magu mkoani Mwanza, Wakili wa serikali kutoka Wizara ya Katiba na Sheria ambaye pia ni mratibu wa mafunzo hayo, Dorice Dario amesema mafunzo hayo ni kuendeleza mkakati wa serikali katika kuwawezesha watumishi umma katika kada zote kutekeleza ipasavyo falsafa ya Rais Samia Suluhu Hassan kuhusu 4R.

Pia amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwakumbusha na kuwajengea uwezo washiriki ili waelewe namna ya kutekeleza majukumu yao kwa kufuata misingi ya utawala bora na haki za binadamu na demokrasia.

"Mafunzo haya ni utekelezaji wa falsafa ya Rais Samia ya ‘Rebuilding’ (kujenga upya) ambapo tunaamini tukimaliza mafunzo haya washiriki wote watakuwa wamejengwa upya uwezo wa kutekeleza majukumu yao kwa ufasaha kwa wananchi,” amesema.

Akifungua mafunzo hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Mohamed Ramadhani amesema dhana ya mafunzo hayo ni kuimarisha utoaji bora wa huduma kwa wananchi.

“Tunatarajia matokeo ya mafunzo haya tuyaone kwa wananchi. Hivyo, tukae tupokee tukayatekeleze ili amani iendelee kutawala kwa wananchi,” amesema.

Akizungumza baada ya kupata mafunzo hayo, Afisa Mtendaji wa kata ya Nkungulu, Sara Kunzugala mbali na kuishukuru Serikali kwa kuwapatia mafunzo hayo, amesema mafunzo hayo yatasaidia kuwa chachu ya mabadiliko katika vituo vya kazi hasa ikizingatiwa wao wanajumuika moja kwa moja na wananchi katika kutekeleza majukumu yao.

“Tumejengewa uwezo wa kuwaelewesha wananchi namna ya kutambua haki zao, kwa hiyo tutatumia mafunzo haya kuwaambia wananchi wasiwe na hofu kudai haki zao na tutawaelekeza njia sahihi za kutekeleza lengo hilo,” amesema.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WADAU WA SANAA MAGU WATAKIWA KUJISAJILI BASATA

    May 07, 2025
  • INEC YARIDHISHWA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA MAGU

    May 03, 2025
  • DC Magu:Wazazi pelekeni watoto wapate chanjo ya polio

    April 30, 2025
  • WAANDISHI, WAENDESHA BVR 136 WALA KIAPO MAGU

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa