• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

DED MAGU AWAFUNDA WATUMISHI WAPYA, AWATAKA KUTAMBUA WANAMUWAKILISHA RAIS

Posted on: March 7th, 2025

Na Mwandishi Wetu, Mwanza

MKURUGENZI wa Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu, Mohamed Ramadhan amewataka watumishi wapya walioajiriwa katika halmashauri hiyo kutambua kuwa wanapotekeleza majukumu yao wanamuwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan hivyo wawahudumie wananchi kwa uweledi.

Pia amewataka watumishi hao kutoa huduma kwa jamii kwa kuzingatia lugha ya staha kwa kuwaelewesha wananchi kuhusu huduma wanazozitoa badala ya kutumia jazba.

Mkurugenzi huyo ametoa kauli hiyo leo tarehe 7 Machi, 2025 wakati akizungumza na watumishi hao wapya walioajiriwa katika halmashauri hiyo kwenye idara mbalimbali ikiwamo, afya, kilimo, sheria na fani nyingine.

“Naomba utambue popote unaposimama kama mtumishi wa umma, unasimama kwa niaba ya Mhe. Rais, ndio maana mwananchi akienda hospitali asipopatiwa matibabu ikitokea akakutana na kiongozi aliyepewa dhamana ya afya atamueleza kuwa hajapatiwa matibabu, kwa sababu kiongozi huyo pia anamuwakilishi Rais, hivyo lazima utambue huo umuhimu.

“Lakini pia ukiingia kwenye jamii hauingii na yale uliyotoka nayo darasani bali unakuwa na principal zako za kuwaelewesha wananchi wakuelewe, inabidi uwashawishi kwa kuangalia faida za pande zote ikiwamo za kiuchumi,” amesema.

Ametoa mfano kuwa fani kama vile wanasheria na madaktari ndio wanaotumia zaidi ya asilimia 80 ya kile walichotoka nacho chuoni na kwenda kutumia kazini.

“Wengine ukienda kwenye jamii usiende mzimamzima lazima uisome jamii ipoje, ila mtu ili aweze kukielewa kitu lazima awe na akili timamu sio kumlazimisha. Ukimshawishi na kumuelekeza na akakuelewa, hata ukitoka ataendelea kutumia kile ulichomuelekeza,” amesema.

 Naye Ofisa Utumishi wa halmahauri hiyo, Henry Sadatale naye amewataka watumishi hao wapya kutambua kuwa malalamiko yoyote yatakayojiri kuhusu watumishi hao tafsiri yake wanaichafua ofisi wanayoitumikia.

“Kuna suala la matumizi ya lugha kwa sababu unaweza kupata jazba… lakini ukimjibu mtu vibaya hiyo ni tofauti na dhamira ya serikali, maana yake ni kwamba umeitukanisha serikali.

“Utoaji huduma lazima uzingatie staha, akija mgonjwa hata lugha tu inamponya. Pia kuna suala la kutunza siri, ni vema kutunza siri kwa sababu badala ya kuwa msuluhishi wa kila jambo unaweza kuleta mtafaruku ambao utaiharibu taswira ya ofisi yako,” amesema.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WADAU WA SANAA MAGU WATAKIWA KUJISAJILI BASATA

    May 07, 2025
  • INEC YARIDHISHWA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA MAGU

    May 03, 2025
  • DC Magu:Wazazi pelekeni watoto wapate chanjo ya polio

    April 30, 2025
  • WAANDISHI, WAENDESHA BVR 136 WALA KIAPO MAGU

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa