• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

DC Magu azindua Rasmi Ujenzi wa Shule Mpya ya Sekondari katika kijiji cha Salama-Bugatu

Posted on: June 3rd, 2020

Mkuu wa wilaya ya Magu Dr. Philemon Sengati (PhD), leo tarehe 02.06.2020 amezindua rasmi ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari kijiji cha salama-Bugatu inayojengwa kwa ufadhili wa Kampuni ya “Alliance Ginnery” inajishughulisha na ununuzi na uchakataji wa zao la Pamba iliyoko katika kijiji cha Kasori Wilaya ya Bariadi Mkoani –Simiyu.

Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya amewasili mapema katika Kiijiji cha Bugatu akiwa ameongozana na kamati ya Ulinzi na Usalama , Mkurugenzi Mtendaji (W), Katibu wa CCM (W), na kupokelewa na maandamo ya mamia ya wananchi wa Kata ya Ng’haya, wakiimba nyimbo za pongezi kwa Serikali iliyodhamiria kwa dhati kuleta maendeleo dhahiri wakionesha kuvutiwa na utendaji bora wa Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Jemedari mkuu Dr. John Pombe Magufuli Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

Meneja wa Kampuni ya “Alliance Ginnery” Ndugu Boaz Ogola, amempongeza Mkuu wa Wilaya ya Magu, Mbunge wa Jimbo la Magu Mhe. Boniventura Kiswaga, Mkurugenzi Mtendaji Wilaya Lutengano Mwalwiba na Diwani wa Kata ya Ng’haya Gerald Paul kupitia vikao mbalimbali waliomba Kampuni kufadhili ujenzi wa Shule ya Sekondari ya pili katika Kata ya Ng’haya ambapo watoto wamekuwa wakisafiri umbali mrefu. “Sasa kampuni imekubali na Mhe: Mkuu wa Wilaya tunakuhakikishia kuwa tunajenga shule hii kwa ubora na kasi kama ilivyo kasi ya Chama Cha Mapinduzi kuleta maendeleo nakuahidi tutakukabidhi Vyumba vinne vya madarasa,jengo la utawala na vyoo matundu kumi. Hii ni kwa muda wa miezi miwili tu”. Amesisitiza Ogola –Meneja wa Alliance Ginnery.

DC. Sengati ameishukuru na kuipongeza Kampuni ya Alliance Ginnery kuwa ni mdau mkubwa wa maendeleo ambaye amejipambanua na anajitambua kwa kuungana na jamii pamoja na Serikali katika shughuli za maendeleo ya jamii. Hivyo basi sura na mwonekano wa wananchi kisaikolojia wamehamasika na mradi huu naamini wako tayari na wako kushiriki kikamilifu.

“Wafadhili wetu mko katika mikono salama na ninawataka wananchi wote kuwa walinzi na washiriki  katika kufanikisha malengo yetu ya kuwaokomboa watoto wetu waliokuwa wakipata shida ya kutembea umbali mrefu km 16 kutoka Salama hadi Ng’haya. Aidha Mhe: Mkuu wa Wilaya amewataka watanzania kujivunia Uongozi wa Rais Magufuli ambao Dunia na Ulimwengu unamheshimu na kumtumainia kama Dira kwa Viongozi wa Dunia na Mzalendo namba moja anayelinda utu, haki na maslahi ya Watanzania na Waafrika kwa ujumla. Pia Mheshimiwa DC amekabidhi mchoro wa ramani ya majengo ya Shule kwa mfadhili na kuwaahidi wananchi kuwa mradi utasimamiwa kwa taratibu zote za Kiserikali na utakuwa mradi wa mfano katika shule zote za Magu.

Dominique Bubeshi Mwakilishi wa Mbunge katika hafla hiyo amesema kuwa Mbunge wa Jimbo la Magu ana imani kubwa na Uongozi wa DC Sengati kuwa ni kiongozi anayeishi maneno yake na kuwa ni mahiri katika wa uhamasishaji na uchangiaji wa maendeleo jimboni.

Afisa Tarafa ya Ndagalu Bi.Grace Msilanga amesema kuwa hii ni ndoto ya muda mrefu ya wananchi ambayo DC Sengati ameitimiza kwa wakati.

Gerald Paul Diwani wa wakati wa Ng’haya amesema kuwa mradi huo ni wa Kata ya Ng’haya hivyo wananchi waupokee na washiriki kikamilifu kadri watavyoombwa kushiriki kwa namna yoyote, “Mimi siyo msemaji bali Mtendaji” Amesema Gerald Diwani wa kata ya Ng’haya.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAGU YAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUENDELEA KUINUA KIUCHUMI KUNDI LA VIJANA

    May 21, 2025
  • MAGU YATENGA MILIONI 92 KUTENGENEZA MADAWATI 1300

    May 21, 2025
  • DC NASSARI AONGOZA KIKAO MAANDALIZI MBIO ZA MWENGE WA UHURU MAGU

    May 21, 2025
  • KILIO CHA MAJI MWAMABANZA KUISHA JUNI 2025

    May 16, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa