• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

Dc Magu Akabidhi Fedha na Pikipiki kwa Vikundi vya Wajasiliamali

Posted on: October 23rd, 2020

Mkuu wa Wilaya ya Magu Mheshimiwa Salum Kalli tarehe 23.10.2020 amekabidhi  fedha na pikipiki 21 kwa vikundi vya wajasiliamali (wanawake Vijana na walemavu), Maafisa Ugani na polisi kama asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri inayorejeshwa kwa wananchi.

DC Magu amempongeza Mkurugenzi Mtendaji (W) na timu yake kwa kutenga fedha kwa ajili ya mikopo ya wanawake, vijana na walemavu “ Hongereni sana kwa kazi mnzaozifanya na muendelee na ushirikiano huo, mimi nimefarijika sana yanayofanyika katika Taifa hili ni makubwa sana kwani Rais Wetu amejipambanua sana katika kuwaletea wananchi maendeleo. Tutawapatia jumla ya pikipiki 21 leo, mkazifanyie kazi iliyikusudiwa na mfikie watu kwa wakati na fedha hizo mlizopewa mkazisimamie vizuri ili ziwe na tija na kuwasaidia” amesema DC Kalli.

Kabla makabidhiano Hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Magu Ndugu. Lutengano George Mwalwiba amesema kuwa kwa Mwaka wa fedha 2019/2020 Halmashauri imefanikiwa kutoa mikopo  kiasi Tshs 210,000,000 kwenye vikundi  vya wanawake, vijana na walemavu kama asilimia 10 ya mapato ya ndani ambayo imetolewa kwa asilimia 100. “kwa Mwaka huu robo ya kwanza pekee tumekopesha vikundi kiasi cha Tshs. 90,000,000”. Amesema kuwa Halmashauri inategemea mapato yake ya ndani kwa 64% kutoka sekta za  kilimo na mifugo ndio maana Menejimenti imeamua kutoa pikipiki 10  kwa Maafisa Ugani. “kwa miaka miwili mfululizo tumekuwa vinara kwenye maonyesho ya wakulima nanenane kanda ya ziwa Magharibi” amesema Lutengano.

Aidha amepongeza kamati ya ulinzi na usalama kwa ushirikiano inaotoa katika kuhakikisha Halmashauri inakusanya Mapato yake na kutokana na mapato hayo Halmashauri imetoa pikipiki 3 kwa Jeshi la Polisi Magu ili ziweze kurahisisha utendaji kazi, kompyuta mpakato 1 katika Ofisi ya TAKUKURU na Ofisi ya Usalama Kompyuta Mpakato 1. Vikundi vya vijana vimepata pikipiki 8 kwa ajili ya uzalishaji.

Wajasiriamali wameshukuru sana kwa mikopo waliyoipata kutoka Halmashauri na wameahidi kushirikiana na Serikali hii ya wamu ya Tano ya Dkt John Pombe Magufuli. Nao Maafisa Ugani wametoa shukrani na kuahidi kuwa wamejipanga kufanya uhamasishaji wa kilimo nyumba kwa nyumba na kijiji kwa kijiji.

Kwa niaba ya Kamati ya ulinzi na usalama OCD Magu Ndugu Mahamoud Banga ameshukuru mkurugenzi na timu yake ya Menejimenti kwa kutoa pikipiki 3 kwa Jeshi la Polisi na Kompyuta Mpakato kwenye Ofisi za usalama na TAKUKURU. Amesema pikipiki zitapelekwa kwenye vituo vya polisi kama ilivyopangwa. Aidha amesema Kaulimbiu ya Kamati ya Ulinzi na usalama Magu inasema “umoja wetu ndiyo Nguvu yetu na nguvu yetu ndiyo umoja wetu”

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WADAU WA SANAA MAGU WATAKIWA KUJISAJILI BASATA

    May 07, 2025
  • INEC YARIDHISHWA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA MAGU

    May 03, 2025
  • DC Magu:Wazazi pelekeni watoto wapate chanjo ya polio

    April 30, 2025
  • WAANDISHI, WAENDESHA BVR 136 WALA KIAPO MAGU

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa