• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

Dc Magu Aanza Kutatua Mgogoro wa Wakulima na Wafugaji Katika Kijiji cha Kisamba

Posted on: November 14th, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Magu Dkt. Philemon Sengati ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama (W) ametangaza kufuta Chama kinachodaiwa kuwa ni cha kutetea Wafugaji katika kijiji cha Kisamba Wilayani Magu. Amefikia uamuzi huo katika Mkutano wa hadhara uliofanyika tarehe 13.11.2018  alipofika katika kijiji hicho kwa lengo la kusikiliza chanzo cha mgogoro uliodumu kwa miaka sita sasa, akiwa katika mkutano huo amehoji uwepo wa wafugaji na chama chao ambacho siku chache alifanya nao kikao Ofisini kwake.

Viongozi  hao wa wafugaji hawakufika katika mkutano huo muhimu uliolenga kutatua mgogoro ambao unatishia amani na usalama kwa Wananchi. Kufuatia kupuuza huko amemhoji Mkurugenzi Mtendaji iwapo Chama hicho kinatambulika kisheria majibu yakawa kuwa hawana chama cha wafugaji na hawajawahi kusajiliwa katika Halmshauri ya Magu. Ndipo Mkuu wa Wilaya akatangaza kukifuta chama hicho na kumwagiza Mkuu wa Polisi wa Wilaya kuwafikisha Ofisini kwake waliokuwa wakijinasibu kuwa ni Viongozi wa Chama Cha Wafugaji ili wajieleze kwani nini wamejivika majukumu hayo kinyume cha sheria.

Mkuu wa Wilaya ameongozana na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wilaya ya Magu, Pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya aliyewakilishwa na Afisa Mtendaji wa Mamlaka ya mji mdogo wa Magu pamoja na Diwani wa kata ya Lubugu Mheshimiwa Lucas Zabron. Wananchi wamelalamikia kijiji chao kuvamiwa na Wafugaji wenye makundi makubwa ya mifugo ambayo inaharibu  mazao ya wakulima kila kukicha na jambo hili limepelekea kuibuka chuki kwa baadhi ya Wakulima wanaoharibiwa mazao yao na kushambuliwa na wachungaji kwa kupigwa na kujeruhiwa.

Vilevile wananchi wamemweleza Mkuu wa Wilaya kuwa Viongozi wa Serikali ya Kijiji wamekuwa vinara wa mgogoro huo kwani huwakaribisha wafugaji na hupatiwa kitu kidogo, na hii ndiyo sababu Wafugaji wamekuwa na kiburi wanadiriki kuchungia katika mashamba ya mazao ya wakulima hata nyakati za usiku, pia wamekuwa na majibu ya kejeli kuwa watakaoendelea kuhoji mifugo katika kijiji hicho wataozea jela, Pia Umoja wao huo ni wa Wafugaji wavamizi lakini wafugaji wenyeji hawashirikishwi katika hicho chama, ndiyo maana hata leo Mheshimiwa DC hawapo katika mkutano wako. Amesema mmoja wa wanakijiji anayedai kuwa ni mhanga wa sakata hilo.


DC Sengati akiwahutubia wananchi hao amewaaambia kuwa anahitaji kuiona Kisamba ikiwa na amani tena amani ya kudumu bila mgogoro, na kwamba sifa ya kuwa na mgogoro wa muda mrefu ni jambo lisilokubalika katika kipindi hiki tunapojielekeza katika ujenzi wa Magu ya mfano Tanzania katika shughuli za kimaendeleo. Pia “Rushwa ni jambo ambalo halina nafasi katika Wilaya ya Magu. 

Pia Viongozi wote tubadilike tutangulize maslahi mapana ya Taifa mbele na siyo maslahi binafsi au kikundi chochote kile hata kama ni cha Matajiri, Sisi tunatekeleza ndoto za Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ya kuwatetea wanyonge na kuhakikisha haki na usawa vinastawi katika Taifa letu. “Niwaalike kwa namna ya pekee kujiepusha na rushwa inayozalisha migogoro kwa uporaji wa haki za wengi,
Mimi sikuja magu kutafuta utajiri hutosikia kuwa nimepokea wala kuomba rushwa. Mwenyekiti wa Kijiji na Serikali yako umetajwa kujihusisha na rushwa ambayo ndiyo kiini cha mgogoro huu tutakuchunguza na kesho saa 2:00 asubuhi ufike Ofisini kwangu na wananchi endeleeni kutupatia ushirikiano na taarifa sahihi kwa kila hatua ili tuweze kuondosha mgogoro huu na kuanzia leo ni maarufuku kwa mfugaji yoyote yule, Kulisha, Kuharibu mazao, kutishia na kuwashambulia wakulima”.

“Pia nakuomba Mkurugenzi wa Wilaya Shughulikieni suala la kuwabaini wafugaji wenye makundi makubwa ya mifugo walivamia na namna walivyoingia, "pia muone namna ya kutenga maeneo ya malisho na mashamba ili atakayeingilia eneo la mwingine sasa tuweze kuanza naye kumshughulikia” amesema Dkt Sengati.

.
Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji akipokea maagizo ya Mheshimiwa DC amesema kuwa ‘ “Tumepokea lakini wananchi mnajua namna mlivyoasisi mgogoro huu, maana wafugaji hawawezi kuja bila ninyi kuwakaribisha, Kwa hiyo tutaona namna bora ni kuwashirikisha wote katika maamuzi, kuondosha hili balaa la Wakulima kulishiwa mazao yao kwa kweli inarudisha nyuma maendeleo yenu wakulima” Amesema Fundikira kwa niaba ya mkurugenzi Mtendaji wilaya.

Magu Kusema na Kutenda.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • PPRA YAWAPIGA MSASA WALIMU WAKUU, WATENDAJI KATA MAGU KUHUSU MATUMIZI MFUMO NeST

    May 27, 2025
  • Mchengerwa aagiza maofisa habari kukabidhiwa ofisi

    May 23, 2025
  • MAGU YAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUENDELEA KUINUA KIUCHUMI KUNDI LA VIJANA

    May 21, 2025
  • MAGU YATENGA MILIONI 92 KUTENGENEZA MADAWATI 1300

    May 21, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa