• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

DC, DED MAGU WAZINDUA KWA KISHINDO ZOEZI LA UANDIKISHAJI UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA

Posted on: October 11th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Magu, Joshua Nassari pamoja na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Mohamed Ramadhani wamezindua zoezi la uandikishaji wananchi katika daftari la wapiga kura wa uchaguzi wa serikali za mitaa kwa kujiandikisha katika vitongoji wanavyoishi.

Katika uzinduzi huo uliofanyika leo tarehe 11 Oktoba mjini Magu mkoani Mwanza, Nassari amejiandikisha katika kituo cha Unyamwezini kilichopo kata ya Itumbili huku Mkurugenzi wa halmashauri hiyo akijiandikisha katika kitongoji cha National kilichopo kata ya Magu Mjini.

Akizungumza baada ya kujiandikisha, Mkuu huyo wa wilaya ametoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kujiandikisha kwa sababu ni zoezi ambalo linafanyika chini ya dakika moja.

“Uandikishaji huu hauna complication (vikwazo) ndani ya dakika moja unajiandikisha kisha unaendelea na majukumu yako pia kuna mawakala wa vyama vyote, usalama na amani ipo ya kutosha.

“Mara nyingi watu wanadhani uchaguzi ni ule wa uchaguzi mkuu tu, lakini huu ni muhimu zaidi kwa sababu hawa ni viongozi ambao wapo na wewe usiku na mchana, ndio viongozi ambao kwa lolote nyumbani kwako anakuwa wa kwanza kufika,” amesema Nassari.

Naye Mkurugenzi wa halmashauri hiyo amesema ametoa wito kwa wananchi kujitokeza kujiandikisha kwa sababu zoezi hilo halihitaji mwananchi kuja na kitambulisho chochote zaidi ya majina kamili kwani wakala anaweza kutambua mkazi wa kitongoji husika.

“Wengine wanasema tayari walijiandikisha mwezi uliopita, ule ulikuwa kwa ajili ya uchaguzi mkuu, na baada ya kujiandikisha orodha itabandikwa kwenye maeneo yote ya wazi hivyo wananchi waende kuhakiki au wale ambao hawastahili kupiga kura waweze kutolewa kisha tuende kwenye awamu nyingine ya uchukuaji fomu za kugombea nafasi mbalimbali,” amesema.

Aidha, baadhi ya mawakala wa vyama vya siasa akiwemo Philemon John (Chadema) na Fausta Anthoni (CCM), wamesema zoezi hilo linafanyika kwa usalama hivyo wananchi wajitokeza kwa wingi kujiandikisha ili kuwa na sifa za kumchagua kiongozi wanayemtaka.

Uzinduzi wa zoezi hilo la uandikishaji ambalo litafanyika kwa siku 10 kuanzia Oktoba 11 hadi 20 mwaka huu, limeenda sambamba na shamrashamra za maandamano yaliyoanzia katika ofisi za wilaya ya Magu hadi uwanja wa Mwanankanda ambako kumefanyika mchezo wa soka kati ya mashabiki wa Simba na Yanga.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • PPRA YAWAPIGA MSASA WALIMU WAKUU, WATENDAJI KATA MAGU KUHUSU MATUMIZI MFUMO NeST

    May 27, 2025
  • Mchengerwa aagiza maofisa habari kukabidhiwa ofisi

    May 23, 2025
  • MAGU YAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUENDELEA KUINUA KIUCHUMI KUNDI LA VIJANA

    May 21, 2025
  • MAGU YATENGA MILIONI 92 KUTENGENEZA MADAWATI 1300

    May 21, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa