• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

Dc Awashukuru Wananchi Kushiriki Usafi wa Mazingira Katika Siku ya Kilele cha Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia

Posted on: December 14th, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Magu Dkt. Philemon Sengati ametoa shukrani hizo katika siku ya kilele cha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia iliyofanyika katika uwanja wa Sabasaba tarehe 13.12.2018. Amesema ” napenda kuwashukuru sana kwa kuhusianisha suala la Ukatili wa Kijinsia na zoezi tulilolifanya la usafi wa mazingira kwa mji wetu wa Magu. Nawapongeza sana wote kwa ushiriki wenu na kuweza kufanikisha siku hii ya leo kuwa pamoja kwa wingi kiasi hiki”.

Aidha amesema Siku hii ya Kupinga ukatili wa Kijinsia  Duniani ni siku ya kutafakari kujua ukatili wa kijinsia ni nini, unafanyika vipi, ni nini madhara yake na namna ya kuzuia ukatili huo usiendelee. Serikali yetu kwa kushirikiana na Wadau mbalimbali itaendelea kuongeza juhudi za kuwezesha suala la utoaji wa Elimu  katika maeneo yote ya Nchi hususani Vijijini. Kauli mbiu ya mwaka huu ni “FUNGUKA, PINGA UKATILI WA KIJINSIA, ELIMU SALAMA KWA WOTE”.

“Magu kama zilivyo wilaya nyingine nchini ni miongoni mwa Wilaya zinazokabiliwa na Ukatili na Unyanyasaji wa Kijinsia miongoni mwa Wananchi kwa kiasi kikubwa. Ukatili huu unaosababisha Madhara mengi kwenye Jamii kiuchumi na Kiafya. Aidha kuna aina mbalimbali za ukatili wa kijinsia kama vile kimwili, Kingono, Kiuchumi na Kiakili/Kisaikolojia” amesema Dkt. Sengati.

Amewaomba Wananchi kutoa ushirikiano kuondoa aina zote za ukatili wa kijinsia na kufikia usawa wa kijinsia ili kuwa na jamii iliyo salama na yenye ustawi. “Hivyo ninawataka wanajamii wote, viongozi wa Madhebu ya Dini na Watendaji wote wa Serikali, kwa ujumla wetu kuhakikisha tunadhibiti vitendo vyote vya unyanyasaji na ukatili wa kijinsia katika Jamii. Hii ikiwa ni pamoja na kuripoti matukio yote ya unyanyasaji na ukatili wa kijinsia yanayotokea katika jamii na kuhakikisha tunatoa ushahidi pindi tukihitajika. Kwa kufanya hivyo tunaweza kuongeza umri wa kuishi wa watu wetu hivyo kuchangia kwa ukamilifu ujenzi wa Taifa.

Mwisho, amewapongeza wadau mbalimbali wanaoendelea kuisaidia Halmashauri yetu katika mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia ambapo amewasisitiza wananchi kuendelea kuifanyia kazi Kauli mbiu ya mwaka huu ya “FUNGUKA, PINGA UKATILI WA KIJINSIA, ELIMU SALAMA KWA WOTE”. Kwa pamoja tunaweza kuzuia ukatili wa kijinsia, tuungane na kuendeleza nchi yetu.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAGU YAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUENDELEA KUINUA KIUCHUMI KUNDI LA VIJANA

    May 21, 2025
  • MAGU YATENGA MILIONI 92 KUTENGENEZA MADAWATI 1300

    May 21, 2025
  • DC NASSARI AONGOZA KIKAO MAANDALIZI MBIO ZA MWENGE WA UHURU MAGU

    May 21, 2025
  • KILIO CHA MAJI MWAMABANZA KUISHA JUNI 2025

    May 16, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa