• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

BARAZA LA MADIWANI MAGU LAIAGIZA TARURA KUTEKELEZA MIRADI KWA WAKATI

Posted on: November 16th, 2024

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Magu limeagiza Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) wilayani Magu kutekeleza miradi ya miundombinu ya barabara yenye changamoto kwa kuhakikisha fedha zilizotengwa kwa ajili ya matengenezo hayo zinatumika ipasavyo.

Hayo yamebainishwa leo tarehe 15 Novemba 2024 na Mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Simon Mpandalume katika Kikao cha Baraza la Madiwani robo ya kwanza kilichofanyika wilayani Magu ambapo Baraza hilo limepokea  taarifa za utekelezaji wa Shughuli za maendeleo ngazi ya Halmashauri kwa kipindi cha mwezi Julai hadi Septemba 2024.

Mwenyekiti huyo amesema madiwani wengi wamekuwa wakipiga kelele kuhusu kusuasua kwa miradi inayogusa taasisi hizo kwa kuwa wakandarasi wanaotekeleza miradi hiyo wamepatikana bila hata kushirikisha mameneja wa wilaya katika taasisi hizo.

 Aidha, Mwenyekiti huyo alisema hivi karibuni halmashauri kwa kushirikiana na jeshi la polisi litaanza kuwasaka wananchi ambao kaya zao hazina choo ili kudhibiti mlipuko wa kipindupindu ambao ulijitokeza katika tarafa ya Ndagalu.

Akikazia kuhusu mlipuko huo wa kipindupindu, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Mohamed Ramadhani alisema baadhi ya kaya zimekuwa zikikaidi kwa makusudi kufuata maelekezo ya watalaam wa afya ambao wamekuwa wakitoa huduma, elimu na tiba kuhusu ugonjwa huo na matokeo yake, mgonjwa katika familia akipona baada ya siku chache  anapokelewa tena mgonjwa toka  kwenye familia ile ile kwa ugonjwa ule ule. Ukifanyika ufuatiliaji ngazi ya familia wataalam hukuta dawa za kutibu maji familia hawazitumii, hawachemshi maji na maji tiririka hayatumiki katika familia hizo.

“Tumezuia mikusanyiko yote hadi minada hakuna chakula kinachouzwa sio hali nzuri lakini inasababishwa na baadhi ya wananchi ambao hawana vyoo na wanaendelea kuwa chanzo cha kusambaza vimelea vya kipindupindu. 

“Watu wana nyumba zilizoezekwa bati za msauzi lakini eti hazina choo"

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAGU YAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUENDELEA KUINUA KIUCHUMI KUNDI LA VIJANA

    May 21, 2025
  • MAGU YATENGA MILIONI 92 KUTENGENEZA MADAWATI 1300

    May 21, 2025
  • DC NASSARI AONGOZA KIKAO MAANDALIZI MBIO ZA MWENGE WA UHURU MAGU

    May 21, 2025
  • KILIO CHA MAJI MWAMABANZA KUISHA JUNI 2025

    May 16, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa