• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

Waziri wa Maji na Umwagiliaji Aagiza Mkandarasi Kukamilisha Mradi wa Maji Magu Mjini Ifikapo Mwezi Februari, 2019

Posted on: August 16th, 2018

Waziri wa Maji na Umwagiliaji Prof. Makame Mbarawa amefanya ziara katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu tarehe 16.08.2018 ambapo ametembelea mradi mkubwa wa maji Magu Mjini na mradi wa kisima kirefu kinachotumia Mfumo wa Jua (Solar) Katika kijiji cha Lubugu. Amesema kwamba, Halmashauri ya wilaya ya Magu imekuwa na changamoto ya ukosefu wa maji ya kutosha kwa muda mrefu ambapo hadi sasa upatikanaji wa maji ni asilimia 23 maeneo ya mjini na asilimia 45 maeneo ya vijijini. “Hivyo Serikali imeleta mradi huu Mkubwa wa maji  pindi utakapokamilika tatizo la maji Magu litakwisha, na mradi huu utagharimu Fedha za kitanzania Billioni 12” amesema Prof. Mbarawa.

Aidha ameagiza Mkandarasi  kukamilisha Mradi huo mkubwa wa maji kufikia Mwezi Februari 2019, japo mkataba unaonyesha mradi utakamilika mwezi Mei, 2019. ”Msimamizi wa Mradi (Consultant) asimamie Mkandarasi masaa 24 kwa siku ili kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati na wananchi wapate huduma ya maji”.

Mbunge wa Jimbo la Magu Mhe. Destery Kiswaga amesema kwamba, ifikapo Mwaka 2019 suala la maji litakuwa historia kwani huu ni utekelezaji wa ilani ya Chama cha Mapinduzi ya Mwaka 2015. “Chanzo cha Maji kilichopo hakiwezi kutosheleza wananchi wote kwa sasa kwani idadi ya watu imeongezeka, mradi uliopo ulijengwa mwaka 1974 pindi watu wakiwa 6000 tu, hivyo wananchi waendelee kuamini Serikali ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania iliyopo Madarakani inayopenda maendeleo Wananchi wake chini ya Dkt. John Pombe Magufuli” amesema Kiswaga. 

Mkuu wa Wilaya ya Magu Dkt. Philemon Sengati amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kumteuwa kuwa mwakilishi wake katika Wilaya ya Magu ambapo, ameahidi kufuatilia shughuli mbalimbali za kimaendeleo na kuhakikisha zinafanyika kwa ufasaha. “Mradi huu mkubwa wa maji utakuwa wa Kihistoria kwani ukikamilika utawaondolea wananchi adha ya maji katika wilaya ya Magu”

Pamoja na mradi huo mkubwa wa maji, Mheshimiwa waziri Prof. Mbarawa ameweka jiwe la ufunguzi wa mradi wa maji katika kijiji cha Lubugu. Amesema kwamba, nia ya Serikali ni kupeleka maji kila eneo la nchi hii hivyo kwa kutambua hilo “Serikali imeamua kujenga mradi huu wa maji unaotumia mfumo wa jua (solar) katika kijiji hichi, hivyo mtumie maji haya na kuulinda mradi huu uendelee kufanya kazi muda mrefu kwani umegharimu kiasi cha fedha shilingi Millioni 193, pia ni mradi wa gharama nafuu katika uendeshaji wake” amesema Prof. Mbarawa. Aidha, ameahidi kufanyia kazi suala kupeleka mradi wa maji wa kutumia mfumo wa Jua katika kijiji cha Sayaka.

Mhe. Waziri wa Maji na Umwagiliaji akipata Maelezo Juu ya utekelezaji wa Mradi Mkubwa wa Maji Magu Mjini

Mhe. Waziri wa Maji na Umwagiliaji akikagua ujenzi wa Mradi wa Maji Magu Mjini

Mhe. Waziri wa Maji na umwagiliaji akichimba Mtaro wa kupitisha bomba la maji

Kaimu Mhandisi wa Maji Magu akieleza Juu ya Mradi wa Kisima Cha kutumia Mfumo wa Jua (solar) Kijiji Cha Lubugu

Mbunge Jimbo la Magu akizungumza na Wananchi wa Kijiji cha Lubugu

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Magu akizungumza na wananchi wa kijiji cha Lubugu

Mhe. Waziri wa Maji na Umwagiliaji akizungumza na Wananchi wa Kijiji cha Lubugu

Uzinduzi wa Mradi wa Kisima cha kutumia mfumo wa Jua (Solar) katika Kijiji Cha Lubugu

Mhe. Waziri wa Maji na Umwagiliaji akimtwisha maji Mwananchi Katika kijiji cha Lubugu baada ya uzinduzi wa Mradi huo


Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAGU YAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUENDELEA KUINUA KIUCHUMI KUNDI LA VIJANA

    May 21, 2025
  • MAGU YATENGA MILIONI 92 KUTENGENEZA MADAWATI 1300

    May 21, 2025
  • DC NASSARI AONGOZA KIKAO MAANDALIZI MBIO ZA MWENGE WA UHURU MAGU

    May 21, 2025
  • KILIO CHA MAJI MWAMABANZA KUISHA JUNI 2025

    May 16, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa