• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

Waziri Azitaka Halmashauri Zote Nchini Kutoa Mikopo Yenye Tija kwa Wanawake

Posted on: March 9th, 2019

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na watoto Mheshimiwa Ummy Mwalimu amezungumza hayo katika siku ya kilele cha Maadhimisho ya  wanawake Duniani  yaliyofanyika kimkoa  katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu kata ya Bujora tarehe  08.03.2019. Amesema maadhimisho haya ya wanawake yalianza rasmi mwaka 1997 ambapo baada ya mwaka 2005 siku ya wanawake huadhimishwa Kitaifa kila baada ya miaka mitano.

Aidha amesema, kaulimbiu ya mwaka huu imezingatia muktadha wa vipaumbele vya nchi yetu ambapo inasema “BADILI FIKRA KUFIKIA USAWA WA KIJINSIA KWA MAENDELEO ENDELEVU” . Utekelezaji wa kaulimbiu hii utawezesha wanawake katika maendeleo hivyo “tuwe na fikra chanya kuhusu nafasi ya Mwanamke, tujitafakari ni jinsi gani atashiriki katika Falsafa ya Tanzania ya Viwanda kuelekea uchumi wa kati. Serikali itaongeza fedha kwenye bajeti ya mfuko wa Wanawake ili waendelee kupata mikopo bila riba” amesema Waziri Ummy.

Amepongeza mkoa wa Mwanza kuunda kamati za ulinzi wa mwanamke na mtoto, aidha amezitaka Halmashauri zote nchini kuunda kamati hizo katika ngazi za wilaya, kata, vijiji na vitongiji. Pia amesema “ni wajibu kila Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri kutenga asilimia 4 kutoka vyanzo vya mapato ya ndani kwa ajili ya kuwasaidia wanawake kiuchumi na mikopo inayotolewa kwa wanawake lazima ihusianishwe na  na kaulimbiu ya Tanzania ya Viwanda. Wanawake wapewe mikopo yenye tija itakayowawezesha kusonga mbele kiuchumi na sio kutoa mikopo ya laki tano”.

Wanawake wasibaki nyuma katika kuomba nafasi mbalimbali za uongozi katika maeneo yao, wabadili fikra na kutojiona wanyonge kifikra. Jamii itokomeze rushwa ya ngono ambapo amewataka wanawake kuwa mstari wa mbele kupeleka malalamiko yao TAKUKURU kama kuna viashiria vya rushwa ya ngono dhidi yao. Wakuu wa shule na Walimu Wakuu waendelee kuwasilisha taarifa ya watoto ambao wameacha shule na kuolewa kila robo kwani maboresho ya Sheria ya elimu lazima itekelezwe amesema Waziri Ummy..

Mwisho amezindua kampeni ya “Simpigi Tena” katika dhana nzima ya kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake. Amempongeza Shetta na kuahidi kuunga mkono juhudi zake ambapo amesihi wadau mbalimbali wajitokeze kuunga mkono Shetta katika kampeni aliyoianzisha ya “Simpigi Tena” . Aidha amemaliza kwa kumshukuru Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwa kuunga Mkono haki za Wanawake.


Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAGU YAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUENDELEA KUINUA KIUCHUMI KUNDI LA VIJANA

    May 21, 2025
  • MAGU YATENGA MILIONI 92 KUTENGENEZA MADAWATI 1300

    May 21, 2025
  • DC NASSARI AONGOZA KIKAO MAANDALIZI MBIO ZA MWENGE WA UHURU MAGU

    May 21, 2025
  • KILIO CHA MAJI MWAMABANZA KUISHA JUNI 2025

    May 16, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa