• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

VIONGOZI WA DINI, SIASA WAPONGEZA MIRADI YA MAENDELEO INAYOTEKELEZWA MAGU

Posted on: November 26th, 2024

Na Mwandishi Wetu

VIONGOZI wa dini, mila na siasa katika Halmashauri ya wilaya ya Magu mkoani Mwanza wameipongeza Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa kupelekea miradi mikubwa ya maendeleo kwenye halmashauri hiyo hatua ambayo imetajwa kuwa itachochea maendeleo ya wananchi wa wilaya hiyo.

Viongozi hao wametoa pongezi na shukrani hizo jana Jumatatu baada ya kutembelea miradi mbalimbali ikiwamo ujenzi wa daraja la Sukuma, Simiyu, jengo jipya la halmashauri na ujenzi wa shule mpya ya sekondari Bundlya.

Ziara hiyo maalumu iliandaliwa na Mkuu wa wilaya ya Magu, Joshua Nassari kwa kushirikiana na Mkurugenzi wa halmashauri, Mohamed Ramadhani.

Akitoa taarifa kuhusu ujenzi wa daraja la Sukuma lililopo kata ya Ng’haya wilayani humo, Mhandisi Hassan Habibu kutoka Tanroad Mwanza, alisema daraja hilo pamoja na barabara unganishi, linajengwa kwa gharama ya Sh bilioni 11.4.

Alisema daraja hilo lenye urefu wa mita 70 na upana wa mita 11 pia litakuwa na barabara unganishi zenye urefu wa km 2.2 ambapo zitajengwa upande wa upande wa Ng’haya na Lumeji.

“Mradi ulianza mwaka jana Oktoba mwaka jana na sasa umefikia asilimia 25 kutokana na changamoto ya mvua kubwa lakini mkandarasi ataongeza speed ndani ya muda mfupi mpaka kufikia Machi mwaka 2025 atakuwa amekamilisha kazi hii,” alisema.

Akitoa pongezi hizo baada ya kutembelea daraja la Sukuma lililopo wilayani Magu, Paroko wa Parokia ya Magu Jimbo kuu la Mwanza, Padre Onesmo Shigelwa alisema madaraja katika wilaya hiyo yamekuwa changamoto kubwa katika shughuli za usafirishaji lakini ujenzi huo unaoendelea umeleta ahueni kwa wananchi.

Naye Sheikh wa wilaya ya Magu, Nuhu Zaid Khamis alisema yanayotendeka katika wilaya hiyo ni tafsiri halisi ya vitabu vya dini kwa namna serikali inavyowajali watu wake.

Mwenyekiti wa Chadema – Magu, Malimi Butage pia aliipongeza serikali kwa miradi hiyo ya maendeleo na kusisitiza kuwa miradi hiyo inaendelea kufungua shughuli za kiuchumi kwa wananchi bila kujali itikadi za kiasiasa.

Naye Mbunge wa jimbo hilo la Magu, Boniventure Kiswaga alisema akiwa kama kiunganishi kati ya Serikali na wananchi, ujenzi wa madaraja hayo ya Sukuma na Simiyu inayogharimu zaidi ya Sh biilioni 60 ni moja ya mambo aliyokuwa akiyapigia kelele bungeni kila mara.

“Kwa sababu mazao yalikuwa yanakwama kwa kukosa vivuko. Barabara hizi pia zimefikia hatua usanifu wa kujenga kwa kiwango cha lami kwenda Bariadi na Mahaha, kinachofuata ni kupata fedha. Pia ujenzi wa ‘round about’ ya kwenda Kwimba serikali imetoa bilioni 14 na mkandarasi ataanza kujenga km 10,” alisema.

Kuhusu ujenzi wa jengo la utawala Kiswaga alisema hivi karibuni serikali imetoa Sh milioni 700 kumalizia ujenzi wa jengo hilo ambalo ndilo litakuwa makao makuu ya halmashauri.

Aidha, Mkurugenzi wa wilaya hiyo, Mohamed Ramadhani alisema muda wowote wanaweza kuhamia kwneye jengo hilo jipya.

“Tunategemea Januari hadi Februari ndani ya jengo kutakuwa kumekamilika, na kubakia nje. Lakini pia ili kurahisishia wananchi kupata huduma hapa, halmashauri imeshatenga fedha, kwa ajili ya stendi na ninawahakikishia jengo hili litakuwa miongoni mwa majengo bora kwani hata mwananchi anayekuja kufuata huduma atapata pia huduma ya intaneti bure,” alisema.

Mkuu wa wilaya hiyo, Joshua Nassari alisema ziara hiyo ililenga kuwaonesha miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali ili waone kwa kwa macho badala ya kuelezwa pekee.

“Tutaendelea kufanya utaratibu wa kushirikisha watu kwani maendeleo ya Magu ni ya wananchi wa Magu,” alisema.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAGU YAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUENDELEA KUINUA KIUCHUMI KUNDI LA VIJANA

    May 21, 2025
  • MAGU YATENGA MILIONI 92 KUTENGENEZA MADAWATI 1300

    May 21, 2025
  • DC NASSARI AONGOZA KIKAO MAANDALIZI MBIO ZA MWENGE WA UHURU MAGU

    May 21, 2025
  • KILIO CHA MAJI MWAMABANZA KUISHA JUNI 2025

    May 16, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa