• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

RC Mwanza awataka Waajiri Wote Katika Mkoa Wa Mwanza Kufuata Sheria na Taratibu za Kazi Kutatua Changamoto za wafanyakazi

Posted on: May 1st, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mheshimiwa John Mongela ameagiza  hayo katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi  Duniani  yaliyofanyika kimkoa katika Halmashauri ya wilaya ya Magu leo tarehe 01.05.2019 katika viwanja vya Sabasaba. Amesisitiza waajiri wote wakiwemo wa makampuni binafsi kukaa na watumishi wao kwa kufuata sheria na taratibu katika suala la kutatua changamoto zinazowakabili wafanyakazi ili kuepuka migogoro inayoweza kujitokeza.

Aidha ametoa wito kwa mifuko ya hifadhi ya jamii kuwa watumishi wanapopeleka malalamiko ya stahiki zao watoe  suluhisho. Maboresho yanayoendelea kufanywa katika mifuko hiyo yawe na lengo la kuwapa amani watumishi wa Umma na sio viginevyo hasa wanaostaafu baada ya kumaliza muda wao wa utumishi. “Lazima maombi ya wafanyakazi yatazingatiwa hivyo, tuendelee kufanya kazi kwa bidii na kauli mbiu inayosema  ‘UCHUMI WA KATI INAWEZEKENA, WAKATI WA MISHAHARA NA MASLAHI BORA KWA WAFANYAKAZI NI SASA’  ninaiunga Mkono kinachohitajika kwa wafanyakazi ni kuwa na Subira pamoja na kufanya kazi kwa mshikamano ” amesema RC Mongela.

“Katika Mkoa wa Mwanza tutahakikisha hakuna haki ya Mfanyakazi inayopotea kwani wafanyakazi wanachangia sana katika kuleta amani na utulivu katika  Mkoa Wetu, kuna baadhi ya maeneo wafanyakazi wanabaguliwa ambapo sio jambo jema kufanya hivyo, katika vikao vyote vya uwakilishi lazima kuwepo na wawakilishi wa vyama vya wafanyakazi ili maazimio ya vikao yanapofikiwa, yawe yanafika sehemu husika nakufanyiwa kazi  na kutekelezwa kwa wakati. Vyama vya wafanyakazi vipo kisheria kwa ajili ya kutatua changamoto za wafanyakazi. Tumuunge mkono Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli ili tusonge mbele katika Maendeleo ya nchi yetu” amesema RC Mongela.

Awali Mwenyekiti wa TUCTA Mkoa wa Mwanza ametoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kukubali kuwa mgeni rasmi katika Maadhimisho ya wafanyakazi yanayofanyika kitaifa Mkoani Mbeya, Mkuu wa mkoa wa Mwanza kuwa Mgeni Rasmi Katika Maadhimisho haya ya Kimkoa hapa Wilayani Magu na Mkuu wa Wilaya ya Magu kwa kufanya Maandalizi mazuri kwa ajili ya siku ya wafanyakazi kimkoa bila kumsahau Mkurugenzi Mtendaji (W) na timu yake. Aidha ametoa changamoto zinazowakabili wafanyakazi wa Mkoa wa Mwanza mbele ya Mgeni rasmi kwa ajili ya kuzipatia ufumbuzi.

Nae Mkuu wa Wilaya ya Magu Dkt Philemoni Sengati (Phd) amewataka wafanyakazi kuwa wazalendo, wafanye kazi kwa bidii na kuepuka mbinu za kizamani za kusuluhisha migogoro, bali watumie Diplomasia kudai haki. Aidha ameshukuru uongozi wa Mkoa kuleta maadhimisho haya ya wafanyakazi ya mwaka 2019 Wilayani magu.


Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MILIONI 250 ZA MFUKO WA JIMBO ZAACHA ALAMA MAGU

    June 09, 2025
  • WAKULIMA MAGU WAMPA TANO KISWAGA KUCHOCHEA KILIMO CHA UMWAGILIAJI

    June 07, 2025
  • KISWAGA AZIPIGA JEKI KATA 12 KWA MIFUKO 1040 YA SARUJI, MADAWATI 130

    June 06, 2025
  • Shule 53 Magu zagawiwa zana za kufundishia wanafunzi wa awali

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa