• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

NASSARI AMREJESHEA TABASAMU MLEMAVU KWA KUMPATIA MGUU BANDIA, MTAJI

Posted on: February 26th, 2025

MKUU wa Wilaya ya Magu mkoani Mwanza, Joshua Nassari amerejesha tabasamu la kijana aliyepata ulemavu wa viungo vya mguu na mkono kwa kumuwezesha kupata mguu bandia pamoja na kiti mwendo (Wheelchair).

Pia kijana huyo Ndalawa Emanuel Maduka (23) ambaye ni mkazi wa Itumbili wilayani Magu, amepatiwa fedha kiasi cha milioni tano zitakazomuwezesha kufungua biashara ya kuuza vipuri vya pikipiki katika eneo hilo.

Msaada huo umekabidhiwa leo tarehe 26 Februari, 2025 na Mkuu huyo wa wilaya mbele ya Mwenyekiti wa taasisi ya Desk and Chair Foundation – Mwanza, Alhaj Dk. Sibtain Meghjee ambao ndio walifadhili wa msaada huo.

Akizungumza katika makabidhiano hayo, DC Nassari aliishukuru taasisi hiyo ya Desk and Chair Foundation kwa kusaidia upatikanaji wa mguu bandia pamoja na fedha hizo za mtaji.

“Tunawashukuru sana, wamekuwa wakisaidia jamii na huyu ni mmoja wa wanufaika wa ufadhiili huu. Tulisema tusimtafutie baiskeli na mguu na kuishia hapo, kwa sababu ana ulemavu wa viungo ila sio wa akili hivyo ataendelea kutumia ile taaluma yake ya ufundi.

“Tutamfungulia biashara ya kuuza spea za pikipiki hapa Magu. Tutaifuatilia kwa karibu, hatutaki mtaji uende kupotea, tunataka tuone anatoka na kunyanyuka kwa sababu akili yake inafanya kazi,” amesema Nassari.

Aidha, Mwenyekiti wa taasisi ya Desk and Chair Foundation – Mwanza, Alhaj Dk. Sibtain Meghjee amesema baada ya kuelezwa uhitaji wa kijana huyo na Mkuu wa wilaya aliguswa na kuanza kwa kutoa kitimwendo.

“Baada ya kupata milioni 5, tulitoa hapo 700,000 ili apate mguu wa bandia. Sasa kilichobaki tumekileta ili apate mtaji. Nipongeze kwa kumpa mafunzo ya ujasiriamali namna ya kusimamia mtaji huu,” amesema.

Akishukuru kwa msaada huo, Mama kijana huyo, Gina Efugomo alisema ataenda kumpa ushirikiano wa kutosha mwanaye huyo ili aweze kusimamia vema mtaji aliopewa.

Naye Ndalawa ambaye alipata ulemavu huo mwaka jana wakati akiwa kwenye majukumu yake ya ufundi wa umeme wa magari, mbali na kumshukuru mkuu wa wilaya pamoja na taasisi hiyo amesema sasa kwa mtaji huo anakwenda kuinuka tena.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WADAU WA SANAA MAGU WATAKIWA KUJISAJILI BASATA

    May 07, 2025
  • INEC YARIDHISHWA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA MAGU

    May 03, 2025
  • DC Magu:Wazazi pelekeni watoto wapate chanjo ya polio

    April 30, 2025
  • WAANDISHI, WAENDESHA BVR 136 WALA KIAPO MAGU

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa