Kiswahili
  • English
  • Kiswahili
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

Naibu Waziri OR-TAMISEMI Aweka Jiwe la Msingi katika Shule ya Sekondari Lumve

Posted on: March 16th, 2018

Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mheshimiwa Joseph G. Kakunda (Mb) amefanya ziara Wilayani Magu na kuweka jiwe la msingi katika shule mpya ya Sekondari Lumve iliyopo kata ya Bujora tarehe 16.03.2018. Amepongeza Jitihada na ushirikiano unaoonyeshwa baina ya Viongozi na wananchi katika kuchangia ujenzi wa shule ya sekondari Lumve.

Amesisitiza kuendelea kushirikisha wananchi katika kuchangia miradi ya maendeleo kwani Serikali haijakataza wananchi kuchangia maendeleo, bali michango yote inayohusiana na maendeleo inatakiwa iratibiwe na Serikali ya Kijiji husika na kupitisha kiwango cha kuchangia kulingana na kaya zilizopo kwa kufuata taratibu zilizopo na sio kuadhibu wanafunzi.

Amesema kuwa, kuna mambo mengi yanayohitajika ili shule ya sekondari Lumve itimize vigezo vya kusajiriwa hivyo viongozi wahakikishe wanasimamia ili majengo mengine kama vile maabara na jengo la utawala yakamilike kwa wakati.

Pia ameshauri viongozi wa vyama vingine vya siasa waunge mkono miradi ya maendeleo katika maeneo yao kwani huu ndio mwelekeo wa Serikali ya awamu ya tano kuwaletea wananchi wake maendeleo. “Serikali imeleta Tshs. 60,000,000.00 ya ujenzi wa Maabara kwa ajili ya kuunga mkono juhudi za wananchi wa Kata ya Bujora” Amepongeza Diwani wa kata ya Bujora kwa kuchangia Tshs. 9,000,000.00 katika ujenzi wa shule ya sekondari Lumve.

Naibu Waziri OR TAMISEMI amepongeza usimamizi mzuri unaofanyika kwa watoto wenye mahitaji maalum katika shule ya msingi Itumbili pamoja na kuwa  shule hiyo maalumu ina changamoto mbalimbali zinazoikabili. Amesisitiza shule hiyo ipewe kipaumbele na kuona utaratibu wa kuongeza shule nyingine zenye mahitaji maalum katika wilaya ya Magu.

Aidha amezungumza na watumishi ambapo amewasisitiza kufanya kazi kwa weledi kwani Serikali ya awamu ya tano imedhamiria kuboresha huduma  kwa wananchi wake katika sekta za elimu, afya na Maji. “Tumuunge Mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwani ana Uthubutu wa hali ya Juu katika kufanya Maamuzi na kutumia Rasilimali za ndani katika kutekeleza miradi mikubwa”. Ushirikiano uliopo uendelezwe kwani kwa kufanya hivyo wananchi watapata maendeleo.

Mhe.Naibu waziri OR TAMISEMI Akiweka Jiwe la Msingi katika Shule ya Sekondari Lumve

Mhe. Naibu waziri OR TAMISEMI Akisikiliza Taarifa ya Ujenzi wa Shule ya Sekondari Lumve

Mhe. Naibu Waziri OR TAMISEMI Akisikiliza Taarifa ya uendeshaji wa Shule ya Watoto wenye Mahitaji Maalum Itumbili

Mhe. Naibu Waziri OR TAMISEMI Akizungumza na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu


Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • PPRA YAWAPIGA MSASA WALIMU WAKUU, WATENDAJI KATA MAGU KUHUSU MATUMIZI MFUMO NeST

    May 27, 2025
  • Mchengerwa aagiza maofisa habari kukabidhiwa ofisi

    May 23, 2025
  • MAGU YAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUENDELEA KUINUA KIUCHUMI KUNDI LA VIJANA

    May 21, 2025
  • MAGU YATENGA MILIONI 92 KUTENGENEZA MADAWATI 1300

    May 21, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa