• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

Naibu Waziri Awataka Waajiri Kutenga Muda wa Kusikiliza Kero za Watumishi Katika Maeneo yao ya Kazi

Posted on: October 4th, 2019

Hayo yamejiri katika ziara ya Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais  Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Dr. Mary Machuche Mwanjelwa iliyofanyika tarehe 03.10.2019  wilayani Magu. Naibu Waziri ameambatana na Baadhi ya Makamishna wa Tume ya Utumishi wa Umma walioteuliwa na Mheshimiwa Rais, Lengo la ziara likiwa ni kusikiliza na kutolea ufafanuzi changamoto zinazowakabili watumishi wa Umma .

Amesema Serikali ya awamu ya tano inawajali, inawapenda na inawathamini watumishi wa Umma na kuwa mtumishi wa Umma ni Fursa na wanahudumia wananchi katika maeneo yao. “kila Mtumishi anatakiwa kupenda na kujali kazi yake kwa nafasi yake aliyonayo, awajibike ipasavyo na kuacha kufanya kazi kwa mazoea katika serikali hii ya awamu ya tano. Waajiri wote Watenge Muda na siku kwa ajili ya kukutana na watumishi wa Umma na kusikiliza kero zao na kuzitatua kwa wakati” amesema Naibu Waziri.

Pia amewataka Watumishi wa Umma kuzingatia Sheria, Taratibu, Kanuni na Miongozo inayotolewa na serikali na kufanya kazi kwa bidii, weledi, umahiri, uzalendo na ubunifu mkubwa katika maeneo ya kazi na kuzingatia  OPRAS kwa vitendo na sio nadharia. “Waajiri watende haki kwa watumishi pindi wanapokuwa na changamoto na kutoa huduma bora kwa wananchi. Suala la Mahusiano kazini ni muhimu sana kwa watumishi waliopewa dhamana ya kuongoza Taasisi. Aidha Barua yoyote inayokwenda nje ya Taasisi lazima ipite kwanza kwa mwajiri wa Taasisi husika”.

Awali Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya Dr. Philemon Sengati amemshukuru sana Naibu waziri kwa kufika kuzungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu na amemhakikishia umoja, Mshikamano na uadilifu uliopo Magu wa kwendana na kasi ya Serikali ya awamu ya tano ya Dkt John Pombe Magufuli. Aidha ameeleza changamoto ya upungufu wa Watumishi katika wilaya ya Magu katika kada mbalimbali.

Nae Mbunge wa Jimbo la Magu Mheshimiwa Destery B. Kiswaga ameshukuru na kupongeza ujio wa Naibu waziri amesema “ katika ziara nilizofanya nimekutana na watumishi wote wa Umma katika tarafa zao wanazofanyia kazi wamenieleza changamoto zao ambapo nyigine zimepatiwa ufumbuzi na nyigine ambazo hazikuweza kupata ufumbuzi nilikuletea na umeshaanza kuzifanyia kazi” amesema Kiswaga.

Mwakilishi wa Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Umma Ndugu John Michael Haule (Balozi) ameeleza kazi mbalimbali zinzofanywa na tume pamoja na watumishi wanaohudumiwa na tume hiyo yenye Makamishina 7 ambapo amesisitiza waajiri kutoa ushirikiano mkubwa katika tume hiyo. Aidha Sekretarieti ya tume hiyo imewasilisha mada ya Misingi ya sheria katika kusimamia haki na wajibu wa watumishi wa Umma.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • PPRA YAWAPIGA MSASA WALIMU WAKUU, WATENDAJI KATA MAGU KUHUSU MATUMIZI MFUMO NeST

    May 27, 2025
  • Mchengerwa aagiza maofisa habari kukabidhiwa ofisi

    May 23, 2025
  • MAGU YAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUENDELEA KUINUA KIUCHUMI KUNDI LA VIJANA

    May 21, 2025
  • MAGU YATENGA MILIONI 92 KUTENGENEZA MADAWATI 1300

    May 21, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa