• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

Naibu Katibu Mkuu apongeza uongozi wa Magu kwa Mshikamano uliopo baina yao na watumishi

Posted on: March 12th, 2020

Naibu katibu mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Gerald Mweli anaeshughulikia elimu ameyasema hayo wakati alipotembelea Halmashauri ya Magu leo tarehe 11.03.2020. akiwa katika ziara amezungumza na uongozi wa wilaya, Maafisaelimu Kata, wakuu wa shule, walimu wakuu pamoja na baadhi ya walimu wa shule za sekondari na msingi katika ukumbi wa shule ya Sekondari Magu.

Amesema “Mahusiano yaliyopo kati ya Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi Mtendaji  (W) na watumishi wengine ni mazuri kwani wanafanya kazi kwa pamoja”. Kuhusu changamoto za  Madaraja na madai mbalimbali kwa watumishi wa umma amesema Serikali inayafanyia kazi ili kila mtumishi alipwe stahili zake.

Amesisitiza kusimamia elimu kwani kipaumbele ni taaluma inayoweza kuleta mapinduzi makubwa katika sekta ya  elimu katika Taifa letu. “Serikali ya awamu ya tano inafanya jitihada kubwa katika suala la kuboresha elimu kwa kujenga miundombinu mbalimbali na zaidi ya shule 250 mpya zimejengwa nchini hivyo viongozi simamieni elimu, taaluma na watumishi waliopo chini yenu na msisite kuchukua maamuzi. Katika suala la changamoto ya upungufu wa walimu wa Masomo ya sayansi na Hisabati endeleeni kutumia walimu waliopo vizuri wakati serikali inajipanga kuajiri walimu wapya” amesema Naibu katibu Mkuu.

Mkurugenzi wa Elimu OR-TAMISEMI Bw Julius Nestory ametoa mwelekeo wa elimu inayopaswa katika kuleta mapinduzi makubwa ambapo amesisitiza sana suala la taaluma, kutumia fedha za miundombinu kwa kuzingatia utaratibu, na maadili kuhusiana na nidhamu za walimu na wanafunzi. “Wakuu wa shule  wafuatilie masomo yanayofundishwa darasani na wasimamie walimu kufundisha mada zote kwa muda na kwa kina”.

Amesema “Msimamizi wa elimu wa awamu ya tano anapaswa kuwasikiliza watu, kufanya maamuzi, kuwa na siri, kuwa na maadili, kufanya kazi zinye matokeo na kuwa mbunifu”. “Maelekezo ya Serikali ni kwamba Maafisaelimu Kata wakae katika vituo vyao vya kazi, kila mkuu wa shule / mwalimu mkuu kufundisha angalau vipindi 4 kwa wiki, maafisaelimu kata na wakuu wa shule angalau wawe na shahada na kukata mshahara kwa walimu  wasiotimiza wajibu wao kwa kutofundisha vipindi vyote” amesema Mkurugenzi wa Elimu OR-TAMISEMI.

Mkuu wa wilaya ya Magu Dr. Philemon Sengati (PhD) ametoa pongezi kwa Naibu katibu mkuu na timu yake kwa kazi anazozifanya za kupunguza changamoto zinazowakabili watumishi. “ watumishi wa wilaya ya Magu ni wachapakazi sana na kwa pamoja tumeanzisha mfuko wa elimu ambapo watumishi wote ni wadau” . amemuomba Naibu katibu mkuu kuchukua changamoto za watumishi hasa madeni na madaraja sambamba na ombi la uanzishaji wa shule za kidato cha tano na sita (A-Level) angalau kila tarafa iwe na shule moja ya aina hiyo.

Awali Mkurugenzi Mtendaji (W) Bw. Lutengano G. Mwalwiba amesema kuwa serikali imekuwa ikitoa mishahara ya watumishi kwa wakati na ametaja mafanikio yaliyotokana na fedha za EP4R tangu mwaka 2016 hadi 2019 katika wilaya ya Magu zilizotumika katika ujenzi wa miundombu mbalimbali ya shule kama vile madarasa 52, mabweni 4 maktaba 1 na matundu ya vyoo vya wanafuzi, utengenezaji wa madawati na kurekebisha ikama ya walimu. Aidha ameomba madai wa walimu  yaliyohakikiwa na kukubalika yafikiriwe ili walimu walipwe kwani ni madeni ya  muda mrefu.

Aidha  amemuomba  Naibu Katibu Mkuu OR-TAMISEMI Kukabidhi vyeti  vya pongezi kwa Mkuu wa wilaya ya Magu, Mbunge Jimbo la Magu, na Idara ya elimu Msingi kwa kutambua jitihada zao katika kuletea Magu Maendeleo. Vile vile  amemuomba kukabidhi mfano wa hundi yenye Jumla ya Tshs. 116,012,255.00  kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kama asilimia 10 inayorudi kwa wananchi kama mkopo bila riba na Naibu waziri amefanya hivyo.

Naibu Katibu Mkuu OR-TAMISEMI Akimpatia DC Magu Cheti cha Pongezi kwa jitihada anazofanya katika kuiletea Magu maendeleo

Naibu Katibu Mkuu OR-TAMISEMI akimpatia Afisaelimu Msingi Cheti cha pongezi kwa kufanya vizuri  katika mtihani wa darasa la saba 2019

Naibu Katibu Mkuu OR-TAMISEMI akikabidhi Mfano wa Hundi yenye Tshs.116,012,255.00 kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAGU YAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUENDELEA KUINUA KIUCHUMI KUNDI LA VIJANA

    May 21, 2025
  • MAGU YATENGA MILIONI 92 KUTENGENEZA MADAWATI 1300

    May 21, 2025
  • DC NASSARI AONGOZA KIKAO MAANDALIZI MBIO ZA MWENGE WA UHURU MAGU

    May 21, 2025
  • KILIO CHA MAJI MWAMABANZA KUISHA JUNI 2025

    May 16, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa