• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

Mkuu wa Wilaya Akagua Shughuli za Ujasiriamali Zinazofanywa na Wanawake

Posted on: March 10th, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Magu Mheshimiwa Khadija Nyembo amekagua shughuli mbalimbali za ujasiriamali zinazofanywa na wanawake katika Maadhimisho  ya siku ya wanawake Duniani yaliyofanyika tarehe 08.03.2018 katika Kata ya Kandawe. Ameahidi kushughulikia changamoto kama zilivyoainishwa katika risala ambapo wilaya itaimarisha  masuala yafuatayo kwa lengo la kuziondoa changamoto hizo;-

Kuendeleza teknolojia ya uhakika wa chakula na lishe.

Kuimarisha program za mafunzo ya lishe bora kwa wanawake, watoto na jamii kama njia ya kinga ya magonjwa nyemelezi.

Kuongeza uelewa kwa wanawake juu ya masuala ya Jinsia

Kuhakikisha kila familia inahifadhi chakula cha kutosha kwa matumizi na ziada.

Kuimarisha huduma za afya na uzazi salama na kuhamasisha wanawake kupima afya zao na kujiunga kwenye mfuko wa afya ya jamii (CHF).

Kuhakikisha wanawake wanashirikishwa katika uongozi wa ngazi zote.

Kuhakikisha Halmashauri yetu inachangia kikamilifu katika mfuko wa maendeleo ya Wanawake na Vijana.

Kuanzisha mtaa wa viwanda vidogo vidogo kwa kushirikiana na Shirika la Viwanda vidogo (SIDO) Mwanza.

Ameendelea kwa kueleza kwamba, Mkakati wa elimu ambao Wilaya imejiwekea ni katika kufanya jitihada za kuondoa hali ya ubaguzi wa aina zote katika jamii, sera ya elimu inahakikisha kuwa, wasichana wanapata nafasi sawa ya kuingia katika mfumo rasmi wa elimu, pia kuwawezesha kuzitumia nafasi hizo kwa ukamilifu zaidi.

Aidha amesema Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yanafanyika kila mwaka kwa kuambatana na kauli mbiu ambayo hutoa mkazo kuhusu jambo fulani. Kauli mbiu ya mwaka huu inasema “KUELEKEA UCHUMI WA VIWANDA TUIMARISHE USAWA WA JINSIA NA UWEZESHAJI WA WANAWAKE VIJIJINI”. “Lengo la kauli mbiu hii ni kuifanya jamii itambue kuwa msingi wa maendeleo katika jamii unachochewa na ushiriki wa mwanamke katika uchumi kwa njia ya viwanda unaoambatana na usawa wa jinsia. Ni jambo la muhimu sana katika kumwendeleza mwanamke na kuondoa unyanyasaji, hivyo tunatakiwa kuendeleza mapambano kwa kasi zaidi na kuzidi kuhamasisha jamii ili kuamsha ari hasa wanaume waendelee kutambua kuwa  wanawake ni washirika wakubwa katika suala zima la maendeleo, hivyo kwa pamoja tunaweza kujenga nchi yetu”.

Amemaliza kwa kusema kwamba, Maendeleo ndani ya wilaya yetu yanaletwa kwa ushirikiano kati ya wanawake, wanaume, serikali na wadau mbalimbali. “Nimefurahishwa  sana kwa kushiriki kwenu  kikamilifu, nina kila sababu  ya kushukuru kwa  ushirikiano wenu”.

Mkuu wa Wilaya ya Magu akipanda mti katika Maadhimisho ya Siku ya wanawake Duniani (chanzo: siku ya wanawake)

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WADAU WA SANAA MAGU WATAKIWA KUJISAJILI BASATA

    May 07, 2025
  • INEC YARIDHISHWA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA MAGU

    May 03, 2025
  • DC Magu:Wazazi pelekeni watoto wapate chanjo ya polio

    April 30, 2025
  • WAANDISHI, WAENDESHA BVR 136 WALA KIAPO MAGU

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa