• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

MAGU YAFANYA KIKAO CHA TATHMINI YA KAMATI YA LISHE, NASSARI ATOA MAAGIZO...

Posted on: March 28th, 2025

Mwenyekiti wa Kamati ya Lishe ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Magu, Joshua Nassari  ameagiza watendaji wa kata kuongeza ubunifu wa kuwashawishi akina mama wajawazito kuzingatia ulaji bora unaojumuisha matunda na mboga za majani vilevile kutumia vidonge vya kuongeza damu ili kuondokana na udumavu kwa watoto na vifo vinavyozuilika kwa akina mama wakati wa kujifungua.

Mkuu wa wilaya ya Magu, Joshua Nassari (katikati) akiongoza kikao hicho. Kulia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Magu, Mohamed Ramadhan na kushoto ni Katibu Tawala wa wilaya hiyo, Jubilate Lawuo.

Pia amewataka watendaji wa kata na vijiji kufanya maadhimisho ya siku ya afya na lishe ya kijiji kwa ajili ya kutoa elimu ya shughuli za lishe kwa wananchi katika Halmashauri ya Magu mkoani Mwanza.

Nassari ametoa maagizo hayo leo Ijumaa tarehe 28 Machi, 2025  katika kikao cha Kamati ya Tathmini ya Lishe kipindi cha robo ya pili Oktoba- Disemba 2024/2025.

Amewataka wajumbe na wakuu wa idara kuendelea na ufuatiliaji na usimamizi wa hali ya lishe katika maeneo yao na kupanda miti ya matunda na mbogamboga kama moja ya njia ya kuhamasisha jamii kuzingatia mlo bora.

"Lakini pia natoa wito mtumie majukwaa mbalimbali ikiwamo ya kidini ili kuwafikia wananchi wengi zaidi katika utoaji wa elimu hii ya lishe," amesema.

Awali Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu, Mohamed Ramadhani ambaye ni katibu wa kamati, amesema tayari halmashauri hiyo imeshaanza kupanda miti ya matunda katika shule mbalimbali ikiwa ni moja ya njia ya kuhamasisha ulaji wa matunda yatakayowasaidia watoto kuondokana na udumavu.

Kwa upande wake Afisa Lishe wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu, Magdalena Lema  wakati akiwasilisha taarifa ya  viashiria vya utekelezaji wa Maendeleo ya shughuli za Lishe Wilayani Magu  na kadi alama,  ameeleza kwamba hali ya utoaji wa Lishe katika shule za msingi na Sekondari imeendelea kuimarika kwa kipindi cha robo ya pili ya mwaka 2024/2025 inayoishia Disemba 2025 na watoto wanaendelea kupata mlo mmoja wakati wa masomo na wazazi na wananchi wamehamasika katika suala la uchangiaji wa chakula mashuleni.

Aidha, amewakumbusha Watendaji wa Kata na Vijiji  wa Halmashauri kufuatilia na kusimamia utekelezaji pamoja na kuhakikisha wanafanya Maadhimisho ya siku ya Afya na Lishe ambayo kwa mujibu wa taratibu na sharia hufanyika mara moja kwa kila robo ya mwaka kwa lengo la kutoa elimu na hamasa ya shughuli za Lishe kwa Wananchi  ili kuweza kufikia malengo ya mkataba wa lishe.

Katika kikao hicho cha Kamati ya Lishe ngazi ya Halmashauri kimewashirikisha Wakuu wa Idara na Wataalam mbalimbali kutoka sekta za afya, elimu, kilimo, na maendeleo ya jamii, pamoja na viongozi wa dini ambao wameahidi kutumia majukwaa yao kuhamasisha mbinu za kupata mlo bora.


Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WADAU WA SANAA MAGU WATAKIWA KUJISAJILI BASATA

    May 07, 2025
  • INEC YARIDHISHWA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA MAGU

    May 03, 2025
  • DC Magu:Wazazi pelekeni watoto wapate chanjo ya polio

    April 30, 2025
  • WAANDISHI, WAENDESHA BVR 136 WALA KIAPO MAGU

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa