• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

DC Magu Akabidhi Tshs. 2,000,000.00 Katika Shule ya Msingi Nyalikungu kwa ajili ya ujenzi wa Vyoo vya Wanafunzi

Posted on: January 25th, 2019

Mkuu wa Wilaya Magu Dkt. Philemon Sengati  amekabidhi fedha kiasi cha Tshs 2,000,000.00 kwa Mwalimu mkuu wa Shule msingi Nyalikungu ambazo zimetolewa na aliyewahi kuwa mwanafunzi wa shule hiyo zaidi ya miaka 30 iliyopita Dr. Stergomena Tax ambaye sasa hivi ni Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo kusini mwa Afrika (SADC).

Dr, Tax ametembelea shule hiyo aliyosoma mwishoni mwa mwaka jana alipokuwa katika mapumziko ya mwisho wa mwaka nyumbani kwake Mtaa wa Unyamwezini, Kata ya Itumbili Wilayani Magu, akiwa ameongozana na Mwanafunzi mwenzie wa miaka hiyo Mzee John Lufega, Dr. Tax baada ya kuona hali ilivyotete katika shule hiyo aliahidi kusaidia ujenzi wa choo shuleni hapo.

Pia amesikitishwa sana kuona vyumba vya madarasa vinane vilivyochakaa na kushindwa kutumika na kupeleka watoto kusoma kwa zamu, Ameahidi pia kufanya ukarabati wa chumba cha darasa alichosomea.

Mkuu wa Wilaya ya Magu ambaye fedha hiyo imetumwa kupitia kwake, akiwa katika kikao cha Wananchi wa Kata Magu mjini na Isandula katika viunga vya shule ya Msingi Nyalikungu,  Amempongeza sana na kumshukuru Katibu Mtendaji wa SADC kwa moyo wake na nia yake ya dhati katika kuisadia jamii ya wanamagu wenzake,” Hakika huyu ni Mtu muhimu kwetu tena ni kiongozi mkubwa lakini alisoma hapa Nyalikungu Shule ya msingi na leo bado anaikumbuka shule yake”

“Tunampongeza sana na nitoe wito kwa Wanafunzi wengine waliowahi kusoma hapa nao warudi waje tuifanye shule hii kuwa shule ya mfano na yenye ubora zaidi hata katika taaluma, ili kuvienzi vipaji vya watu waliopata maarifa S/M Nyalikungu maendeleo ni watu na sisi ndiyo tunawajibika kufanya kazi ili kujiletea maendeleo”. Amesisitiza Dkt Sengati.

Wananchi waliofika katika Mkutano huo wa makabidhiano wamemshukuru sana Dr.Tax kwa uzalendo wake, na hata hivyo Mkuu wa Wilaya Dr. Sengati ameamua kumuunga mkono kwa kuendesha harambee ya kuongezea fedha hiyo ili ikidhi kujenga vyumba 12 vya matundu choo,  amechangia Tsh. 200,000, Lutengano Mwalwiba DED- Magu amechangia Tsh. 100,000, Afisa Elimu Msingi Tsh. 200,000, Mashaka Mathias Diwani Magu mjini Tsh. 100,000, Velina Emmanuel (Diwani Kata ya Isandula) ametoa tripu 1 ya mchanga, Walimu wote wa Shule msingi Nyalikungu nao wamechangia na wananchi wote ambapo Mheshimiwa DC Sengati ameagiza watendaji wa kata kuratibu fedha hizo zilizochangwa na kuzikabidhi shuleni hapo kwa ajili kazi iliyokusudiwa.

Diwani wa kata ya Magu mjini Mheshimiwa Mashaka Mathias amemshukuru Mheshimiwa DC Sengati kwa uaminifu na uadilifu mkubwa alionao katika kuitumikia wilaya yetu, Pia amesema kwa niaba ya Wanamagu “tunampongeza sana Dr. Tax kwa mchango huu na kwamba tunazitumia fedha hizi kwa kazi iliyokusudiwa”.

 Naye Mwalimu Mkuu Beatrice Ngula baada ya kukabidhiwa fedha hizo amewashukuru viongozi kwa mshikamano walio uonyesha katika kusimamia shughuli za maendeleo shuleni hapo, na kwamba wanampongeza sana katibu Mtendaji kwa msaada aliotoa kwa ajili kuisaidia shule ya Nyalikungu ili iendelee kutoa elimu kwa wengine.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAGU YAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUENDELEA KUINUA KIUCHUMI KUNDI LA VIJANA

    May 21, 2025
  • MAGU YATENGA MILIONI 92 KUTENGENEZA MADAWATI 1300

    May 21, 2025
  • DC NASSARI AONGOZA KIKAO MAANDALIZI MBIO ZA MWENGE WA UHURU MAGU

    May 21, 2025
  • KILIO CHA MAJI MWAMABANZA KUISHA JUNI 2025

    May 16, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa