• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

DAS MAGU AWAFUNDA WAGANGA KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025

Posted on: July 16th, 2025

KATIBU Tawala Milaya ya Magu, Zuberi Said Zuberi amewataka waganga wa tiba asili wanaofanya shughuli zao katika wilaya hiyo kudumisha amani pamoja na kuzingatia wajibu wao wa kujisajili ili wapate vibali vitakavyowawezesha kutambulika kisheria.

Pia amewaomba kushirikiana na serikali katika mchakato mzima wa uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu ikiwa ni pamoja na kuhamasisha jamii kushiriki uchaguzi huo.

DAS Zuberi ametoa wito huo jana tarehe 15 Julai, 2025 mjini Magu katika mafunzo ya siku moja yaliyoshirikisha waganga zaidi ya 100 kwa lengo la kuwaelimisha kuhusu umuhimu wa kushirikiana katika kutunza amani na kuepukana na ramli chonganishi.

“Ni haki ya msingi kufanya shughuli ya uganga, lakini haki ina wajibu, bila wajibu ni fujo… mtu kufanya shughuli hii bila kibali ni kwamba anakwenda tofauti na taratibu. Kwa sababu ninyi mnashughulikia na jamii moja kwa moja.

“Kuna takribani waganga 700 katika wilaya ya Magu, lakini waliojisajili ni 409, kwa hiyo kama mkihudumia watu watatu kwa mwezi ni sawa na watu 1,227 ambao mmewahudumia, ni wengi sana lakini mkitaka kutendewa haki mjue wajibu wetu kuzingatia taratibu,” amesema na kuongeza.

“Uchaguzi ni mchakato, ulianza muda mrefu ikiwemo kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura, rai yetu kwenu ni kuwaomba kuhamasisha watu kushiriki uchaguzi, tuwe mabalozi wa kutoa hamasa kuhusu suala la ushiriki wa uchaguzi,” amesema.

Naye Mkuu wa Polisi Wilaya ya Magu - Mrakibu Mwandamizi wa Jeshi la Polisi SSP, Haji Makame aliwaonya waganga hao kuacha kutumia maabara za ramli chonganishi.

“Kufanya ramli ndio kunatuletea shida ndani ya wilaya yetu. Vitu vya msingi tunavyowataka ni kwamba mtoe taarifa kwa sababu haiwezekani mtu atoke Kenya au Tanga aje kufanya vitu vya ajabu Magu alafu ninyi mkae kimya, mkimtaja tukamdhibiti mapema na wilaya yetu itaendelea kuwa shwari. Tunajua wapo wanaokuja wanajificha kwenye vi-gesti nawahakikishia tunafuatilia tutawakamata mmoja mmoja,” amesema.

Mwenyekiti wa waganga wilaya ya Magu, Malale Mirambo aliahidi kusimamia utekeleza wa maagizo yote yaliyotolewa kwao na kuwataka waganga wenzake kwenda kujisimamia.

“Kila kata wajisimamie wenyewe, ambaye hataki kujiunga na umoja wetu kwa kukata kibali rasmi, ninawaomba polisi mkamateni mpelekeni ndani.

“Ninaagiza waganga wote waliopo ndani ya Magu, kama hauna kibali kuanzia jumatatu ijayo ahame kwenye wilaya ya Magu, kwa sababu lazima tutakukamata,” amesema.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • KWAHERI JOSHUA NASSARI, KARIBU DC LAWUO

    July 16, 2025
  • DAS MAGU AWAFUNDA WAGANGA KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025

    July 16, 2025
  • VIJANA MAGU WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA ZA MIKOPO INAYOTOLEWA NA HALMASHAURI

    July 16, 2025
  • WALIMU 120 AJIRA MPYA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI MAGU

    July 10, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa