• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA MAPENDEKEZO YA BAJETI BILIONI 65 MWAKA WA FEDHA 2024/2025

Posted on: January 27th, 2024

Baraza la madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Magu limepitisha kwa kauli moja mapendekezo ya rasimu ya mpango na bajeti kwa mwaka wa fedha 2024/2025 ambapo Halmashauri Ya Wilaya ya Magu iliomba kuidhinishiwa jumla ya Sh Bilioni 65 ( 65,039,205,291.04) kutoka vyanzo vyake mbalimbali na kutoka ruzuku ya Serikali kuu.

Akiwasilisha rasimu ya mpango wa bajeti kwa mwaka fedha 2024/2025 Kaimu Afisa mipango Wilaya ya Magu, Christa D. Manyala alitaja jumla ya Tsh. Bilioni 65 ( 65,039,205,291.04) kati ya fedha hizo Bilioni 1.4 ( 1,492,740,064.00) mapato ya ndani, Bilioni 3.2 (3, 223,327,677.04) za matumizi mengineyo, Milioni 10.5 (10,536,000.oo) za mishahara kutoka mapato yandani, Bilioni 45.8 (45,820,693,800.00) ruzuku ya mishahara, Bilioni 13. (1,310,320,000.00) matumizi mengineyo Bilioni 7.2 ( 7,210,144,000.00 miradi ya maendeleo ya serikali na Bilioni 5.9 ( 5, 971,443,759.00) miradi ya maendeleo ya wahisani ambapo jumla kuu ni shilingi Bilioni 65.


Amesema bajeti kuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Magu kwa mwaka wa fedha 2024/2025 imeongezeka kwa asilimia 20 na mapato ya ndani yameongezeka kwa asilimia 3.10 ukilinganisha na bajeti ya mwaka 2023/2024.


Kwa upande wake Mweneykiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu Simon Mpandalume amemshukuru Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh. Dkt. Samia Suluhu Hasssan kwa kuendelea kupeleka fedha nyingi kwaajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika Wilaya hiyo ikiwemo ujenzi wa shule mpya , zahanati na barabara ambazo zimekua chachu ya maendeleo katika Wilaya ya Magu.


Naye Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu Bi. Fidelica Myovella amesema vipaumbele vya bajeti kwa mwaka wa fedha 2024/2025 vitazingatia mwongozo uliotolewa na kuvitaja vipaumbele vya Halmashauri katika bajeti hiyo ambavyo ni kuboresha huduma za afya, kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunza na kuongeza ufanisi na utendaji kazi.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAGU YAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUENDELEA KUINUA KIUCHUMI KUNDI LA VIJANA

    May 21, 2025
  • MAGU YATENGA MILIONI 92 KUTENGENEZA MADAWATI 1300

    May 21, 2025
  • DC NASSARI AONGOZA KIKAO MAANDALIZI MBIO ZA MWENGE WA UHURU MAGU

    May 21, 2025
  • KILIO CHA MAJI MWAMABANZA KUISHA JUNI 2025

    May 16, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa