• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

WAKULIMA MAGU WAMPA TANO KISWAGA KUCHOCHEA KILIMO CHA UMWAGILIAJI

Posted on: June 7th, 2025

KATIKA kutekeleza kwa vitendo lengo la Rais Samia Suluhu Hassan la kuinua sekta ya umwagiliaji kwa asilimia 50 ifikapo 2030, Mbunge wa Magu, Boniventura Kiswaga ametoa msaada wa pampu kwa wakulima wa kikundi cha Bustani kwa ajili ya kuboresha shughuli za kilimo cha umwagiliaji.

Kikundi hicho kilichopo katika Kijiji cha Kabale kata ya Jinjimili wilayani Magu mkoani Mwanza, kinaendesha shughuli za kilimo cha umwagiliaji kwa kuzalisha mazao ya nyanya na mahindi.

Akikabidhi msaada wa pampu hiyo yenye thamani ya Sh milioni 1.5 leo Jumamosi katika ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Magu – Ilungu kwa niaba ya Kiswaga, Diwani wa Kandawe, Lucas Bomoa (CCM) amewasisitiza wakulima hao kuitunza pampu hiyo na kuongeza uzalishaji wa mazao yao kama walivyomuomba mbunge huyo pindi alipowaahidi kuwasaidia.

Akipokea pampu hiyo kwa niaba ya wanakikundi wenzake ambao jumla wapo 10, Katibu wa Kikundi cha Bustani, Maduhu Manyilizo mbali na kumshukuru mbunge huyo kwa kutekeleza ahadi ya msaada huo wa kikundi, ameahidi kwenda kuongeza uzalishaji kutokana na urahisi wa umwagiliaji walioupata.

“Tuna jumla ya hekari tatu za kilimo cha umwagiliaji, lakini tulikuwa tunamudu kulima hekari mbili tu, sasa kwa msaada huu tutaweza kulima zote tatu na kuongeza mazao yetu ambayo ni nyanya na mahindi. Tunamshukuru sana mbunge wetu kwa msaada huu kwa sababu awali tulikuwa tunatumia ndoo kumwagilia ila sasa pampu hii itakuwa msaada mkubwa kwetu katika kukuza shughuli hizi za kilimo cha umwagiliaji,” amesema.

Katika kipindi cha mwaka 2015 hadi 2020, Serikali iliboresha miundombinu ya umwagiliaji nchini, hivyo kuongeza eneo linalomwagiliwa kutoka hekta 461,000 mwaka 2015 had kufikia hekta 694,715 mwaka 2020.

Hata hivyo, Kwa mujibu wa Mpango Kabambe wa Taifa wa Umwagiliaji wa mwaka 2002 (The National Irrigation Master Plan) Tanzania ina eneo la hekta milioni 29.4 zinazofaa kwa kilimo cha umwagiliaji.

Kati ya hekta hizo, hekta milioni 2.3 zinauwezekano mkubwa wa kumwagiliwa, hekta milioni 4.8 zinauwezekano wa kati na hekta milioni 22.3 zina uwezekano mdogo wa kumwagiliwa.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WANANCHI NYASHIMBA WAISHUKURU HALMASHAURI MAGU UJENZI WA ZAHANATI, SHULE

    June 13, 2025
  • MAGU YATENGENEZA MADAWATI 1300 KWA FEDHA ZA MAPATO YA NDANI

    June 12, 2025
  • MILIONI 250 ZA MFUKO WA JIMBO ZAACHA ALAMA MAGU

    June 09, 2025
  • WAKULIMA MAGU WAMPA TANO KISWAGA KUCHOCHEA KILIMO CHA UMWAGILIAJI

    June 07, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa