• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

RAS MWANZA AIPONGEZA MAGU KUPATA HATI INAYORIDHISHA KWA MIAKA 3 MFULULIZO

Posted on: June 18th, 2025

Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza, Balandya Elikana ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Magu kwa kupata Hati inayoridhisha ya Mdhibiti na Mkaguzi mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa miaka mitatu mfululizo.

Pia ameitaka Menejimenti ya halmashauri hiyo kuja na mpango wa kufuta ufaulu wa daraja la nne na sifuri kwa wanafunzi ili kuhakikisha dhamira ya serikali ya kuboresha elimu inafikiwa kwa wanafunzi kupata daraja la kwanza.

Balandya ametoa maagizo hayo jana tarehe 17 Juni, 2025 wakati akiongoza baraza maalum la hoja za CAG kwa halmashauri hiyo kuishia Juni 30, 2024 kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa, Said Mtanda.

Awali akiwasilisha taarifa ya ukaguzi mbele ya baraza hilo, Kaimu Mkaguzi Mkuu wa Nje Mkoa wa Mwanza, Henry Chausa amebainisha kuwa 2023/24 halmashauri hiyo ilikaguliwa na kupata hati inayoridhisha na kwamba kuna hoja 46 ambazo zinafanyiwa kazi na kufungwa.

Baada ya kupokea taarifa hiyo Balandya amesisitiza hoja zote ambazo hazijatekelezwa ziwekewe mkakati wa utekelezaji wake ili zifungwe.

“Hivyo naagiza muweke vielelezo na viambatanisho vyote ndani ya muda ili kuifanya halmashauri ibaki salama,” amesisitiza Katibu Tawala.

Akizungumzia hoja kuhusu ufaulu kwa mwaka 2021-2023, katibu tawala huyo ameitaka menejimenti ya Magu kufuta kabisa daraja sifuri.

“Naomba tukajifunze kwenye halmashauri zingine wanafanyaje kuinua ufaulu mathalani Kwimba twendeni tuone wao wamewezaje kwani mazingira yetu hayatofautiani," amesema Balandya.

Ameongeza kuwa madiwani na watendaji ni wazazi na walezi hivyo wana wajibu wa kuwafundisha stadi za maisha watoto kama kufanya usafi wa mazingira na miili yao ili kuwafanya wawe na utayari na kujenga tabia ya kujitegemea.

Hata hivyo, Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Magu, Simon Mpandalume akichangia hoja hiyo, amefafanua kuwa tayari menejimenti ya halmashauri hiyo imeshafanikiwa kuongeza madarasa mapya, kujenga shule mpya ili kukabiliana na tatizo la utoro wa wanafunzi waliokuwa wanatembea umbali mrefu kufika shule.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • RAS MWANZA AIPONGEZA MAGU KUPATA HATI INAYORIDHISHA KWA MIAKA 3 MFULULIZO

    June 18, 2025
  • WANANCHI NYASHIMBA WAISHUKURU HALMASHAURI MAGU UJENZI WA ZAHANATI, SHULE

    June 13, 2025
  • MAGU YATENGENEZA MADAWATI 1300 KWA FEDHA ZA MAPATO YA NDANI

    June 12, 2025
  • MILIONI 250 ZA MFUKO WA JIMBO ZAACHA ALAMA MAGU

    June 09, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa