• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

SAMIA APONGEZA MAANDALIZI TAMASHA LA BULABO, ATOA UJUMBE KUHUSU MAADILI

Posted on: June 21st, 2025

Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amewataka

Watanzania kushiriki kikamilifu kulinda maadili kwa ajili ya ustawi wa jamii kwa kuwa jukumu

hilo ni la Watanzania.

 

Rais Dkt. Samia ameyasema hayo leo Jumamosi wakati wa ufunguzi rasmi wa Tamasha la Utamaduni la Bulabo lililofanyika katika viwanja vya Bujora-Kisesa, Wilayani Magu.

 

Aidha, Rais Dkt. Samia amesemna Serikali inatambua na kuthamini juhudi kubwa zinazofanywa na wadau wa utamaduni pamoja na viongozi wa kimila katika kuhakikisha utamaduni wa Tanzania unaenziwa na kurithishwa kizazi hadi kizazi.

 

Vilevile, Rais Dkt. Samia ameeleza Serikali inatambua umuhimu wa matamasha ya utamaduni na itaendelea kuyatumia katika kudumisha na kuendeleza utamaduni, mila na desturi za Watanzania.

 

Rais Dkt. Samia ameongeza kuwa utamaduni ndio msingi mkuu wa utambulisho na mshikamano wa Taifa hususan katika kipindi hiki cha mabadiliko ya dunia katika nyanja za kiteknolojia, kiuchumi, kijamii na kiutamaduni.

 

Halikadhalika, Rais Dkt. Samia ameeleza kuwa Serikali inaendelea na juhudi za kuhakikisha Tamasha la Bulabo linatangazwa na kutambulilka kimataifa kutokana na upekee wake katika kuhifadhi utamaduni.

Aidha, Rais Dkt. Samia amewapongeza waandaaji wa Tamasha la Utamaduni la Bulabo la mwaka huu kwa maandalizi mazuri yaliyovutia wageni kutoka mataifa mbalimbali yakiwemo Oman na Jamhuri ya Afrika Kusini, na hivyo kulifanya tamasha hili kuanza kusikika kimataifa.

 

Katika hatua nyingine, Rais Dkt. Samia amepongeza jitihada za Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kuendesha mafunzo sambamba na Tamasha hilo kuhusu umuhimu wa kulinda na kudumisha maadili, mila na desturi za Kitanzania, na kueleza kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kurithisha utambulisho na tamaduni za Taifa kwa vizazi vijavyo.

 

Mapema kabla ya kufungua Tamasha, Rais Dkt. Samia alitembelea Kituo cha Utamaduni cha Bujora na Makumbusho ya Kabila la Wasukuma na kuzungumza na Machifu na Watemi wa kabila hilo.

 

Rais Dkt. Samia amnewaomba viongozi wa kimila, Machifu na Watemi kuendelea kuliombea Taifa liendelee kuwa na amani, umoja na mshikamano wa Taifa.

 

Rais Dkt. Samia amehitimisha rasmi ziara yake ya kikazi mkoani Mwanza na kuwashukuru wananchi wote wa Mkoa huo kwa ushirikiano mkubwa na ukarimu waliomuonesha wakati wote wa ziara yake ya kikazi mkoani humo.

 


Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • SAMIA APONGEZA MAANDALIZI TAMASHA LA BULABO, ATOA UJUMBE KUHUSU MAADILI

    June 21, 2025
  • RAS MWANZA AIPONGEZA MAGU KUPATA HATI INAYORIDHISHA KWA MIAKA 3 MFULULIZO

    June 18, 2025
  • WANANCHI NYASHIMBA WAISHUKURU HALMASHAURI MAGU UJENZI WA ZAHANATI, SHULE

    June 13, 2025
  • MAGU YATENGENEZA MADAWATI 1300 KWA FEDHA ZA MAPATO YA NDANI

    June 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa