• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

RC MWANZA AWAALIKA WALIOKOSA ELIMU RASMI KUJIUNGA NA MPANGO WA ELIMU YA WATU WAZIMA

Posted on: September 15th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ametoa wito kwa wananchi wote wenye umri wa kuanzia miaka 18 ambao wamekosa elimu ndani ya mfumo rasmi kutumia fursa ya uwepo wa vituo vya elimu ya watu wazima kupata maarifa na ujuzi.

Ametoa wito huo mapema leotarehe 15 Septemba, 2025 akiwa katika uwanja wa Sabasaba Wilayani Magu kwenye kilele cha maadhimisho ya juma la Elimu ya watu wazima na elimu nje ya mfumo rasmi Mkoa wa Mwanza.

Amesema, Mkoa huo una zaidi ya watu 262,500 ambao hawajui kusoma na kuandika na kwamba serikali imeanzisha vituo katika Halmashauri zote nane ambapo kuna zaidi ya wanafunzi 36,000wanaopatiwa elimu nje ya mfumo rasmi hivyo ni fursa ya kukimbilia kwa wote waliokosa.

Mhe. Mtanda amebainisha kuwa elimu ya watu wazima inajumuisha programu mbalimbali ikiwemo MEMKWA ambayo ni maalumu kwa ajili ya kuwawezesha waliokosa elimu ya msingi kupata stadi za kujua kusoma, kuhesabu na kuandika ili kufuta ujinga.

Aidha, amebainisha kuwa ndani ya mfumo huo kipo kipengele cha MUKEJA ambacho kinatoa fursa ya kutoa maarifa kwa uwiano ambapo jamii inapewa stadi za ujuzi mbalimbali za ujasiriamali na akabainisha kuwa kuna zaidi ya wafungwa 300 mkoani humo wanapatiwa elimu hiyo. 

Vilevile, ametumia wasaa huo kumshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fursa kwa vijana walioondolewa kwenye mfumo rasmi kwa sababu mbalimbali kama mimba, kupata tena nafasi ya kusoma na kutimiza malengo yao.

Akitoa taarifa ya Mkoa Dkt. Onesmo Nyamweru amesema juma jilo linaadhimishwa kila mwaka karibu na tarehe 8 Septemba kwa kuwa ndiyo siku ya kisomo cha kimataifa duniani kote na kwamba maadhimisho hayo yanatoa fursa ya kutafakari dhana na maendeleo ya Programu za elimu ya watu wazima kupitia maendeleo ya teknolojia. 

"Elimu nje ya mfumo rasmi kitaifa imepanda kutoka 78% hadi 83% na kwa Mwanza wanaojua kusoma na kuandika ni 85.6% elimu hii ni nyenzo muhimu ya kupambana na umasikini, ujinga na maradhi na inakidhi mahitaji ya watu wazima ya sasa kwa jamii iliyo katika shughuli za uzalishaji mali,” amesema Dkt. Nyamweru.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Magu, Jubilate Lawuo akikaribisha wageni waalikwa katika maadhimisho hayo, ametoa wito kww wananchi wa wilaya hiyo ambao walikosa elimu ndani ya mfumo rasmi kuchangamkia mpango huo ambao umekuwa chachu ya maendeleo ya jamii hususani vijana waliopata changamoto mbalimbali ikiwamo mimba za utotoni.


Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • RC MWANZA AWAALIKA WALIOKOSA ELIMU RASMI KUJIUNGA NA MPANGO WA ELIMU YA WATU WAZIMA

    September 15, 2025
  • UTEKELEZAJI SHUGHULI ZA LISHE MAGU WAVUKA 100%

    September 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKEWA MAGU WAZINDUA MIRADI YA BIL. 2

    August 27, 2025
  • ZOEZI LA UTOAJI FOMU LASHIKA KASI JIMBONI MAGU, VYAMA NANE VYAJITOKEZA

    August 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa