• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

MILIONI 250 ZA MFUKO WA JIMBO ZAACHA ALAMA MAGU

Posted on: June 9th, 2025

ZAIDI ya Sh milioni 250 zilizotolewa na mfuko wa jimbo wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu kwa kipindi cha miaka mitano (2020-2025), zimetajwa kuchochea kasi ya maendeleo ya miradi mbalimbali ikiwemo ya afya, elimu, miundombinu na kuunga mkono juhudi za wananchi katika uibuaji wa miradi hiyo.

Hayo yamebainishwa leo Jumatatu na Mbunge wa Magu, Boniventura Kiswaga katika kikao cha kuhitimisha ziara za kukagua miradi iliyotekelezwa na mfuko huo wa kuchochea maendeleo ya jimbo (CDFF).

Katika kikao hicho kilichofanyika kwenye ofisi za halmashauri ya Wilaya ya Magu zilizopo Ilungu, pia kilienda sambamba na kukabidhi kompyuta ya kisasa pamoja na kichapishi (printer) vilivyokabidhiwa kwa uongozi wa shule ya sekondari Kitumba.

Amesema fedha hizo zimeimarishaji ujenzi wa miundombinu mbalimbali ikiwamo ujenzi wa shule za msingi, sekondari na zahanati na nyumba za watumishi.

“Kwa mwaka huu pekee tumesambaza Sh milioni 84 ambazo tumepokea kutoka serikali kuu na kuifanya jumla ya fedha za mfuko wa jimbo kwa miaka mitano kuwa Sh milioni 250 ambazo zimetumika kusambaza vifaa mbalimbali kama mabati kwa ajili ya kuezeka  zahanati, shule za msingi, sekondari na nyumba za watumishi.

“Tumejitahidi kupeleka kwenye vitu vinavyoonekana kama inavyoelekezwa. Tumechangia vya kutosha kwa kuunga mkono pia juhudi za wananchi. Tumpongeze Rais Samia Suluhu Hassan kwani ameleta fedha nyingi kukamilisha uibuaji wa miradi hii ya wananchi huku halmashauri nayo ikichangia asilimia 40 kupitia mapato yake ya ndani,” amesema.

Akizungumza msaada huo wa kichapishi na kompyuta kwa shule ya sekondari Kitumba, Kiswaga amesema aliona vipaji vya wanafunzi katika moja ya mahafali aliyohudhuria shuleni hapo hivyo kuamua kuwaunga mkono wanafunzi hao ili kuendeleza vipaji vyao vya uchoraji.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Magu, Mohamed Ramadhani, Afisa Mipango wa wilaya ya Magu, Pastory Mukaruka amesema kupitia mfuko huo wa jimbo wamegawa vifaa mbalimbali vinavyokwenda kuchochea maendeleo kwenye jimbo hilo ikiwemo kuhamasisha wananchi waendelee kuchangia maendeleo yao.

Awali akizungumza kwa niaba ya wazazi, Mwenyekiti wa bodi wa shule ya sekondari Kitumba, Obedi Mwinula amemshukuru mbunge huyo pamoja na Rais kupitia halmashauri kwa namna anavyoboresha sekta ya elimu kwa ujumla.

Naye Mkuu wa shule sekondari Kitumba, Thomas Yakwala amesema vifaa walivyopatiwa vinakwenda kuleta chachu hasa ikizingatiwa mtaala ulioboreshwa unataka mwanafunzi ajifunze na kutoka shule akiwa na uwezo wa kujiajiri.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MILIONI 250 ZA MFUKO WA JIMBO ZAACHA ALAMA MAGU

    June 09, 2025
  • WAKULIMA MAGU WAMPA TANO KISWAGA KUCHOCHEA KILIMO CHA UMWAGILIAJI

    June 07, 2025
  • KISWAGA AZIPIGA JEKI KATA 12 KWA MIFUKO 1040 YA SARUJI, MADAWATI 130

    June 06, 2025
  • Shule 53 Magu zagawiwa zana za kufundishia wanafunzi wa awali

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa