• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

MAGU YAZINDUA ZOEZI LA UCHOMAJI MASALIA YA PAMBA

Posted on: November 23rd, 2024

MKUU wa Wilaya ya Magu, Joshua Nassari amezindua rasmi zoezi la ung’oaji na uchomaji wa masalia ya pamba na kuwataka wakulima wa zao hilo katika wilaya hiyo kutekeleza zoezi hilo kwa ukamilifu kwani hatosita kuwachukulia hatua za kisheria wale watakaokaidi kuchoma.

Pia amewataka maofisa ugani, watendaji wa kata na vijiji kusimamia zoezi hilo la uchomaji wa masalia ya pamba pamoja na kuhakikisha mbegu pamoja na viuatilifu vinavyotolewa na serikali vinawafikia wakulima ambao ndio walengwa wakuu.

Nassari ametoa maagizo hayo leo tarehe 22 Novemba 2024 mjini Magu wakati akizundua zoezi hilo la uchomaji masalia ya pamba ambalo limeratibiwa na Balozi wa pamba nchini, Agrey Mwanri.

Zoezi hilo lilifanyika sambamba na semina elekezi kwa maofisa ugani, watendaji wa kata, vijiji na maofisa ushirika kwa lengo la kuhakikisha elimu hiyo ya uchomaji wa masalia inawafikia wakulima kikamilifu.

Nassari amesema hatosita kutumia sheria ya pamba iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2011 kufuatilia zoezi hilo na kwa wakulima ambao watashindwa kuchoma masalia hayo watafikishwa mahakamani kwa mujibu wa sheria.

“Kuhusu zoezi hili, sirudi nyuma kwa sababu ni suala la kisheria lakini ni jambo ambalo linakwenda kumnufaisha mwananchi mwenyewe na lengo kubwa ni kumpeleka kwenye mafanikio,” alisema.

Naye Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo, Mohamed Ramadhani amewataka maofisa ugani, watendaji wa kata na vijiji kuwajengea uelewa wa kutosha wakulima kuhusu ulimaji sahihi wa zao la pamba badala ya kurudia kila mara namna ya kupanda zao hilo na namna ya kutumia viuatilifu.

“Hii ni changamoto ambayo inawasumbua sana wakulima wetu kwa sababu tangu miaka ya 1970 wakulima wetu wamekuwa wakifundishwa namna ya kupanda kwa mpangilio na kupulizia viuatilifu… hatupigi hatua kuelekea kwenye mambo mengine, kila mra ni kurudia kilekile, hivyo nawaomba watendaji mhakikisha elimu hii inawafikia kikamilifu badala ya kurudia tena mwakani kuwafundisha,” amesema.

Naye Balozi wa pamba Tanzania, Agrey Mwanri amesema hii ni mara ya pili anatoa elimu kwa wakulima wa Magu kuhusu umuhimu wa kung’oa masalia ya pamba na amebaini kuwa ni wakulima wachache waliochoma masalia hayo kwa mwaka huu.

“Ninachokuomba mhe. Mkuu wa wilaya ni hili suala la uchomaji wa masalia yap amba kwa sababu ni jambo linalotakiwa kusimamiwa kikamilifu. Tangu tarehe 15 Septemba wakulima walitakiwa kuchoma masalia hayo, serikali nayo iliongeza muda hadi Oktoba 15 lakini hadi sasa wakulima hawa hawajachoma.

“Na usipochoma masalia hayo ndipo unaposababisha wadudu kuvamia shamba lako katika msimu unaofuata na kupungua mavuno yako ndio maana tunawasisitiza kuchoma. Pia wasichanganye zao hili la pamba na mazao mengine. Kwa mfano mahindi yanatumia siku 90 kukomaa, lakini pamba siku 150 kwa hiyo ni uhalisia kwamba pamba itanyonywa na mahindi hivyo kukotostawi kwa ubora unaotakiwa,” alisema.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAGU YAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUENDELEA KUINUA KIUCHUMI KUNDI LA VIJANA

    May 21, 2025
  • MAGU YATENGA MILIONI 92 KUTENGENEZA MADAWATI 1300

    May 21, 2025
  • DC NASSARI AONGOZA KIKAO MAANDALIZI MBIO ZA MWENGE WA UHURU MAGU

    May 21, 2025
  • KILIO CHA MAJI MWAMABANZA KUISHA JUNI 2025

    May 16, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa