• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

MAGU YAZINDUA PROGRAMU JUMUISHI YA MALEZI, MAKUZI NA MAENDELEO YA MTOTO

Posted on: February 15th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Magu Mh. Rachel Kassanda amezindua programu ya malezi , makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto (PJT MMMAM) katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu ikiwa na lengo la kukabiliana na kutokomeza changamoto zinazoonekana kuwa ni kikwazo cha hatua sahihi za ukuaji timilifu wa mtoto kimwili, kiakili na kijamii.

Akizungumza wakati akizindua programu hiyo leo Alhamisi Febuari 15 , 2024 DC Kassanda ametoa rai kwa Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu na idara zote zinazotekeleza program hii kwa kushirikiana na wadau kuzingatia utekelezaji Programu hii kwenye maeneo yao kupitia maelekezo na ushauri utakaokuwa na unaotolewa mara kwa mara.


Amesema Uzinduzi huu unafanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu ikiwa ni maelekezo ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum kuwa Programu hii izinduliwe ngazi zote kuanzia Taifa, Mkoa hadi Halmashauri.


"Uzinduzi huu uambatane na utekelezaji wake kwa kuweka Mipango Kazi na kusaidia utengaji wa bajeti na kutoa fedha kwa utekelezaji; amesema "

Kwa upande wake Afisa ustawi wa jamii Wilaya ya Magu, Coretha Sanga amesema kuwa Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi, Makuzi, na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (PJT MMMAM), inayotekelezwa kuanzia 2021/22 hadi 2025/26, inakusudia kuharakisha upatikanaji wa matokeo chanya ya maendeleo ya awali ya mtoto.



Ameongeza kuwa Programu za malezi jumuishi nchini Tanzania zinahitaji kupewa kipaumbele na msisitizo, kutokana na kukosekana kwa uratibu mzuri.


Naye Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu Bi. Fidelica Myovella amesema Halmashauri imejipanga kutekeleza programu hiyo kwa kushirikiana na wataalamu na wadau na kufanyia kazi maelekezo na ushauri uliotolewa na Mkuu wa Wilaya ili kufikia malengo ya utekelezaji wa programu hiyo.


Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • PPRA YAWAPIGA MSASA WALIMU WAKUU, WATENDAJI KATA MAGU KUHUSU MATUMIZI MFUMO NeST

    May 27, 2025
  • Mchengerwa aagiza maofisa habari kukabidhiwa ofisi

    May 23, 2025
  • MAGU YAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUENDELEA KUINUA KIUCHUMI KUNDI LA VIJANA

    May 21, 2025
  • MAGU YATENGA MILIONI 92 KUTENGENEZA MADAWATI 1300

    May 21, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa