• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

MAGU YAJIPANGA KUTOA HUDUMA YA MIGUU BANDIA KWA GHARAMA NAFUU

Posted on: October 2nd, 2024

HALMASHAURI ya Wilaya ya Magu mkoani Mwanza kwa kushirikiana na Taasisi ya Global Peace Network (GPN) pamoja na Tanzania Home Economics Organization- TAHEA), inatarajia kuanza kutekeleza mradi wa utengenezaji wa viungo bandia ikiwamo mikono na miguu ili kuwezesha watu wenye uhitaji wa viungo hivyo kuvipata kwa bei nafuu nchini.

Mradi huo ambao ni wa kwanza kuanza kutekelezwa nchini, unatarajiwa kuanza Machi mwaka 2025 kwa kutengeneza miguu bandia 100.

Akiwasilisha taarifa 2024 kuhusu mradi huo leo tarehe 2 Oktoba, mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Magu, Joshua Nassari, Mkurugenzi Mkuu wa GPN, Dk. Brian Budgell amesema tayari taasisi hiyo imeanza kutoa mafunzo kwa Watanzania ili kuwa na utaalamu wa kutengeneza viungo hivyo.

“Wataalam waliopatiwa mafunzo namna ya kutengeneza viungo hivyo wametoka sehemu mbalimbali huku wakiwa na taaluma zao mathalani uuguzi au udaktari hivyo anajengewa uwezo wa kutengeneza viungo bandia na namna ya kutoa mazoezi tiba,” amesema.

Amesema kutoka Magu wanafunzi saba wamepatiwa mafunzo hayo, Mbeya wanafunzi watatu wamehitimu, Ilemela ni wanne, Kigoma saba na Dar es Salaam watano.

Mbali na utengenezaji wa viungo hivyo, pia wahitimu hao wamepatiwa mafunzo ya utoaji mazoezi tiba hususani kwa wagonjwa wenye matatizo ya kupooza au kiharusi pamoja na magonjwa mengine.

Aidha, Mratibu wa Mradi huo kutoka Hospitali ya Wilaya ya Magu, Sonia Nyamanga amesema mafunzo hayo yamekuwa chachu wa wananchi wa wilaya hiyo hasa ikizingatiwa huduma za mazoezi tiba ni za gharama na huhitaji mgonjwa muda mwingine mgonjwa kufuatwa.

Naye Mratibu wa miradi wa taasisi hiyo ya GPN nchini, Kahenga Mawe amesema ushirikiano mzuri wanaoupata kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Magu kwa zaidi ya miaka 15 sasa, umechangia taasisi hiyo kuendelea kutoa huduma za elimu na afya kwa wananchi.

“Tumefanya tathmini katika hopsitali ya Bugando mguu bandia unauzwa Sh 2.7 milioni, CCBRT na KCMC Sh 2.5 milioni, Ajima wanatoa kwa 700,000, lakini ni matumaini yetu halmashauri ya Magu itatoa huduma hii kwa kiwango Rafiki Zaidi,” amesema.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Magu, Joshua Nassari ametoa wito kwa watumishi wote wa halmashauri hiyo pamoja na wakuu wa idara kutoa ushirikiano wa kutoka katika kutekeleza mradi huo hasa ikizingatiwa ni chanzo kimojawapo cha mapato ya halmashauri hiyi.

“Kwanza niwahakikishie ushirikiano wa kutosha kutoka kwetu sisi viongozi kwa sababu huu ni mradi ambao unakwenda kuwakomboa wananchi wetu hasa wa vijijini ambao hawana uwezo wa kupata viungo hivi bandia, lakini pili niwaagize watumishi wenzangu kutoa ushirikiano wa kutoka kwa mradi huu wa kipekee,” amesema.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • PPRA YAWAPIGA MSASA WALIMU WAKUU, WATENDAJI KATA MAGU KUHUSU MATUMIZI MFUMO NeST

    May 27, 2025
  • Mchengerwa aagiza maofisa habari kukabidhiwa ofisi

    May 23, 2025
  • MAGU YAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUENDELEA KUINUA KIUCHUMI KUNDI LA VIJANA

    May 21, 2025
  • MAGU YATENGA MILIONI 92 KUTENGENEZA MADAWATI 1300

    May 21, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa