• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

KAMATI YA FEDHA MAGU YARIDHISHWA NA UJENZI WA STENDI ILUNGU, SHULE BUNDILYA

Posted on: April 16th, 2025

KAMATI ya Fedha, Uongozi na Mipango ya Halmashauri ya Wilaya ya Magu imeeleza kuridhishwa na utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa stendi ya Ilungu pamoja na shule mpya ya sekondari Bundilya ambayo ujenzi wake umefikia asilimia 95.

Hayo yamebainishwa leo Jumatano wilayani Magu mkoani Mwanza katika ziara ya kamati hiyo inayoongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri, Simon Mpandalume kwa lengo la kujionea maendeleo ya ujenzi wa miradi hiyo.

Akiwasilisha taarifa kuhusu ujenzi wa stendi Ilungu, Msimamizi wa mradi huo, Philipo Justine amesema ujenzi umefikia hatua ya boma na inayofuata ni kupaua boma hilo.

Amesema hadi sasa wametumia zaidi ya Sh milioni 73 kati ya Sh milioni 130 walizopatiwa huku mradi huo ukitarajiwa kutumia Sh milioni 165 fedha ambazo zinatolewa katika mapato ya ndani ya halmashauri.

Naye Msimamizi wa mradi wa shule mpya ya sekondari Bundilya iliyopo Kijiji cha Bundilya kata ya Kahangara wilayani Magu, James Ndega ameieleza kamati hiyo kwamba mradi huo ambao umefikia asilimia 95, unatarajiwa kuanza kusajili na wanafunzi 75 wa kidato cha kwanza.

Mbali na kutaja faida za mradi huo kuwa ni pamoja na kupunguza umbali mrefu wa wanafunzi kutembea, amesema ujenzi wake ambao ulianza Oktoba mwaka jana tayari umetumia kiasi cha Sh milioni 538.

Aidha, Afisa Elimu Sekondari Magu, Beatrice Balige amesema tayari walimu wanne wameletwa kwa ajili ya kuanza kufundisha katika shule hiyo ambayo inatarajiwa kukamilika baada ya mwezi mmoja.

Akizungumzia miradi hiyo, Mpandalume mbali na kueleza kuridhishwa na ujenzi wake, amemuagiza mkurugenzi wa halmashauri kutangaza nafasi za ujenzi wa vibanda vya biashara kwa wananchi ili waanze kujenga katika eneo hilo la stendi kwa mujibu wa ramani ya mhandisi wa halmashauri.

Pia ametoa wito kwa viongozi kuhamasisha wazazi wawalete watoto wao wasome katika shule hiyo mpya hasa ikizingatiwa sasa hakutakuwa na visingizio vya wanafunzi kutembea umbali mrefu.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WADAU WA SANAA MAGU WATAKIWA KUJISAJILI BASATA

    May 07, 2025
  • INEC YARIDHISHWA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA MAGU

    May 03, 2025
  • DC Magu:Wazazi pelekeni watoto wapate chanjo ya polio

    April 30, 2025
  • WAANDISHI, WAENDESHA BVR 136 WALA KIAPO MAGU

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa