• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
MAGU DISTRICT COUNCIL
MAGU DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Magu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Orodha ya viongozi Waliopita
      • Wenyeviti wa Halmashauri
      • Wakurugenzi
      • Wakuu Wa Wilaya
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Kilimo , umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Utumishi na utawala
      • Idara ya Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Fedha
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ugavi
      • Kitengo cha Tehama
      • Internal Audit Unit
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
      • Bujora
    • Miundombinu ya Umwagiliaji
  • Huduma
    • Afya
    • Maji
    • Elimu
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
      • Wajumbe wa Baraza la Madiwani
      • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya UKIMWI (CMAC)
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya vikao vya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Maeneo ya uwekezaji
    • Bajeti
      • 2016/2017 Budget
    • TASAF
    • Mpango Mkakati
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • sheria
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari

DC MAGU AWAFUNDA WENYEVITI WA VIJIJI, VITONGOJI KUELEKEA UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA

Posted on: October 4th, 2024

MKUU wa Wilaya ya Magu mkoani Mwanza, Joshua Nassari amewataka wenyeviti na vitongoji na vijiji katika wilaya hiyo kuhakikisha uchaguzi wa serikali za mitaa unafanyika kwa amani, utulivu na kudumisha umoja kwa masilahi mapana ya Taifa.

Mkuu wa wilaya hiyo ametoa wito huo jana tarehe 3 Oktoba 2024 mjini Magu wakati akizungumza na wenyeviti hao kutoka vijiji 82 na vitongoji 508 vya wilaya hiyo.

Amesema asili ya uchaguzi ni sawa na vita ambayo kila upande huvutia upande wake, lakini kwa vilevile wenyeviti hao ambao wanamaliza muda wao nao watagombea, pindi ikitokea wameshindwa wakubali matokeo badala ya kuibua makundi yasiyokuwa na msingi ndani ya wilaya hiyo.

“Unapofika wakati wa uchaguzi ni sawa na vita, hivyo hata katika nafasi ya ubunge, mbunge wetu (Boniventura Kiswaga) inapotokea mtu amechukua fomu kuwania nafasi yako katika uchaguzi mkuu wa mwakani, usikasirike kwa sababu watu wanaona kazi kubwa uliyoifanya,” amesema.

Katika uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika Novemba 27 mwaka huu, Nassari amewaahidi wenyeviti hao kuwa licha ya uongozi wao kutarajiwa uvunjwa Oktoba 25 mwaka huu kuelekea kwenye uchaguzi huo, hakuna jasho la mwenyekiti yeyote litakalopotea.

Aidha, akizungumza katika mkutano huo, Mbunge wa jimbo hilo, Boniventura Kiswaga (CCM) aliwapongeza wenyeviti hao kwa kuwa kielelezo bora cha kuleta maendeleo kwa wananchi hasa ikizingatiwa wao ndio wasimamizi wa miradi inayoelekezwa na serikali kwenye maeneo yao.

Pia amewaonya wenyeviti hao ambao wengine watatetea nafasi zao, kuzingatia kuwa matokeo ya uchaguzi huo yatatokana na namna walivyokuwa wamejenga mahusiano mazuri na wananchi na sio utekelezaji wa miradi ya maendeleo pekee.

“Lakini pia mnaweza kujitetea kwa sababu kupitia kwa Rais Samia Suluhu Hassan hakuna kijiji ambacho hakijaguswa na miradi ya maendeleo, kuanzia maji, ujenzi wa zahanati na hata barabara,” amesema.

Amesema asilimia 98 ya wenyeviti hao wanaweza kutetea nafasi zao iwapo watajieleza vizuri kwa wananchi hivyo ni lazima kusimama na kushinda uchaguzi huo kwa heshima.

Naye Afisa Uchaguzi wilaya ya Magu, Mwagala Masunga amesema zoezi la kuandikisha wapiga kura uchaguzi huo litaanza tarehe 11 hadi 20 Oktoba mwaka huu huku kampeni zikitarajiwa kuanza tarehe 20 hadi 26 Novemba mwaka huu.

“Tunatarajia zaidi ya wananchi 215,000 wataandikishwa na kuwa na sifa za kupiga kura katika uchaguzi huu, msisitizo ni kwamba kila mtu ajiandikishe kwenye kitongoji chake,” amesema.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAJINA YA WAANDISHI NA WAENDESHA VIFAA WALIOTEULIWA KATIKA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA II April 28, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA HALMASHAURI YA WILAYA YA MAGU ENEO LA ILUNGU NA IGUDIJA TAREHE 02/12/2024 December 01, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA November 18, 2022
  • FOMU ZA KUJIUNGA SHULE YA WASICHANA YA MKOA WA MWANZA MWANZA GIRLS SS 2023 December 16, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WADAU WA SANAA MAGU WATAKIWA KUJISAJILI BASATA

    May 07, 2025
  • INEC YARIDHISHWA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA MAGU

    May 03, 2025
  • DC Magu:Wazazi pelekeni watoto wapate chanjo ya polio

    April 30, 2025
  • WAANDISHI, WAENDESHA BVR 136 WALA KIAPO MAGU

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Serikali yatoa Matrekata 33 katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • Fomu ya Kusafiri nje ya Kituo cha kazi
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Fomu ya Opras
  • Fomu Mpya ya Maombi ya Likizo kwa watumishi
  • Fomu ya Quotation ya likizo
  • Taratibu za mikutano na uendeshaji shughuli za Halmashauri
  • Mwongozo wa Uwekezaji Mkoa wa Mwanza
  • Utaratibu wa kutoa Leseni ya Biashara

Viunganishi Linganifu

  • Wakala ya Serikali Mtandao.
  • Wizara ya Afya
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti kuu ya serikali
  • Ofisi ya Taifa ya takwimu Tanzania
  • tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Haki zote zimehifadhiwa